b..

B1

Wynem

animation

Thursday, March 31, 2011

WAZIRI NCHIMBI AANZA KUONGEA NA WASANII

Mheshimiwa Dr. Emmanuel Nchimbi(pichani), Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo atakutana na wasanii katika ukumbi wa BASATA kuanzia tarehe 31 Machi na tarehe 01 Aprili 2011.Waziri amepanga kuwaona wasanii kwa utaratibu ufuatao:-
31/03/2011 (Alhamisi) Saa 5:00 asubuhi 
Wasanii wa Sanaa za Picha Jongevu na Sanaa za Maonyesho
Saa 7:00 Mchana 
Wasanii wa Sanaa za Muziki na Sanaa za Ufundi
01/04/2011 (Ijumaa)Saa 3:00 asubuhi 
Wasanii wa Muziki wa Kizazi kipya
Izingatiwe kwamba Waziri atawaona wasanii wa muziki kwa siku mbili tofauti. Tarehe 31/03/2011 ataongea na wasanii wa Muziki wote isipokuwa wale wa Kizazi Kipya. Wasanii hao ni pamoja na wale wa Muziki wa Bendi, Taarab, Disco, kwaya na Muziki wa Asili.
Tarehe 01/04/2011 ataongea na wasanii wa muziki wa kizazi kipya tu. Viongozi wa Mashirikisho ya Sanaa hakikisheni wasanii wamepata taarifa na kuhudhuria kwa wakati.
Lengo kuu ni kuongelea maendeleo ya fani za sanaa.
Ghonche Materego
KATIBU MTENDAJI

No comments:

Post a Comment