b..

B1

Wynem

animation

Friday, November 13, 2015

MABONDIA HAMISI MWAKINYO NA MESHACK MWANKEMWA KUPIGANA KESHO JUMAMOSI


Promota Shomari Kimbau akiwainua mikono juu mabondia Asha Nzowa kushoto na Joyce Awino baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao kesho


Bondia Hamisi Mwakinyo kushoto akitunishiana misuli na Meshach Mwankemwa baada ya kupima uzito leo kwa ajili ya mpambano wao wa ubingwa wa taifa unaotambuliwa na  Kamisheni ya ngumi za kulipwa Tanzania TPBC utakaofanyika kesho katika ukumbi wa CCM Mwijuma Mwananyamala katikati ni promomota kutoka katika kampuni ya Golden boy Afrika Shomari Kimbau akiwa na mkanda utakaogombaniwa Picha na SUPER D BOXING NESW



NA Mwandishi Wetu

MABONDIA Meshack Mwankemwa na Hamisi Mwakinyo wamepima uzito kwa ajili ya mpambano wao wa ubingwa wa kg 66 unaotambuliwa na kamisheni ya ngumi za kulipwa nchi mkanda uho uliokuwa umeachwa wazi na bondia Selemani Zogo kwa kuto utetea kwa wakati sasa utapiganiwa na mabondia hawo kesho
akizungumza wakati wa upimaji wa uzito promota wa mpambano uho Shomari Kimbau amesema mkanda uho utapiganiwa na mabondia hawo ili apatikane bingwa mpya wa uzito wa kg 66
mpambano uho utasimamiwa na kamisheni ya ngumi za kulipwa nchini chini ya rais wake Chauremba Palasa aliongeza kwa kusema mbali na mpambano uho siku hiyo pia kutakuwa na ngumi za utangulizi za mabondia mbalimbali
Said Mayanga atamenyana na Gido Selemani wakati Mohamed Amir atapambana na Hemed Hemed
na mpambano mwingine wa kusisimua utakuwa ni wa akina mama ambapo bondia mnaschachali Asha Nzowa 'Asha Ngedere' atapambana na Joyce Awino ambambao ambao unasubiliwa kwa hamu kubwa na mashabiki wanawake wa mchezo wa masumbwi.
Katika mpambano huo siku hiyo kutakuwa na uzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi  kali pamoja na kutambua sheria zake zikiwa na mabondia wakali kama vile

Floyd Mayweathar,Manny Paquaio, Saul 'canelo' alverez ,Mike Tyson,Mohamed Ali,Ferex Trinidad,Miguel Cotto na wengine wengi
pia kuta kuwa na vifaa vya mchezo vitakaokuwa vikitolewa na Kocha Rajabu Mhamila 'Super D' kwa mabondia watakaofanya vizuri siku hiyo na vingine kuuzwa kwa pesa taslimu na kocha huyo kwa ajili ya kuamasisha

Rais wa Kamisheni ya ngumi za kulipwa nchini TPBC Chaurembo Palasa akiwakumbusha baadhi ya sheria zitakazo tumika katika mchezo wa ngumi utakaofanyika kesho katika ukumbi wa CCM Mwijuma Mwananyamala Dar es salaam

Sunday, November 1, 2015

WIZ KID AFUNIKA LEADERS CLUB

Msanii kutoka Nigeria, Wiz Kid Akifanya mambo jukwaani kwenye viwanja vya Leaders Club.
Msanii kutoka Nigeria, Wiz Kid Akifanya mambo jukwaani kwenye viwanja vya Leaders Club.
Msanii kutoka Nigeria, Wiz Kid akiimba huku akiwa nyuma ya jukwaa ikiwa ni muda mfupi kabla ya kupanda jukwaani. 
Msanii Fid Q akiwaburudisa mashabiki wa muziki waliohudhuria tamasha la Wiz Kid, msanii kutoka Nigeria
Msanii Christian Bella kaifanya yake jukwaani.
Msanii wa Filamu nchini, Ray Kigosi akimtunza msanii Christian Bella alivyokua akiimba katika tamasha la Wiz Kid jana.
Msanii Diamond Akiwapa burudani wakazi jiji la Dar na mashabiki wake katika shoo ya Wiz Kid iliyofanyika kwenye viwanja vya Leader Club. 
Sehemu ya mashabiki wa muziki waliohudhuria tamasha la Wiz Kid, msanii kutoka Nigeria
Mc wa Tamasha na mtangazaji wa kituo cha televisheni cha EATV, Sam Missago akifanya yake
Dj Sinyoritha.
Dj Sinyoritha akiwa na mgeni wake kwenye Mashine

Saturday, October 31, 2015

WIZ KID AZUNGUMZIA SHOO YAKE YA LEO USIKU

Msanii Wiz Kid akiwasili katiktika viwanja vya ukumbi wa Solomins kwa ajili ya kuzungumza na waandishi wa Habari
Msanii Wiz Kid akisalimiana na Mratibu wa Tamasha la msanii huyo, King Solomins
Msanii Wiz Kid akitembea kuelekea ndani ya ukumbi wa Solomins kwa ajili ya kuzungumza na waandishi wa Habar
Mratibu wa Tamasha la Wiz Kid, King Solomins akizungumza na waandishi wa Habari akielezea kuhusu shoo nzima ya Wiz Kid itakayofanyika leo katika Viwanja vya Leaders Club.
Msanii Wiz Kid akizungumza na waandishi wa Habari akielezea kuhusu shoo nzima atakayoifanya leo usiku katika Viwanja vya Leaders Club.
Picha zote na Sule Junior

Friday, October 30, 2015

Wapigaji vyombo wa WizKid wawasili

Wakiingia katika basi tayari kwa msafara
Watumiaji mbalimbali wa vyombo vya muziki wa msanii Wizkid wakiwasili katika Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere tayari kwa shoo yao ya leo katika Viwanja vya Leaders.
Huyo mwenye fulana nyeusi anaitwa  Snipes ndio kiongozi wa bendi ya msanii Wizkid
Wakiwa Uwanjani hapo ambapo wameahidi kufanya shoo kubwa wakishirikiana na msanii huyo.  

Wednesday, October 14, 2015

WATOTO YATIMA WA KITUO CHA VALENTINE CHILDREN HOME WAPIMWA AFYA ZAO

watoto wakiwa katika folerni ya kupimwa afya

Muhudumu wa afya ya baba mama na mtoto wa kituo cha alafa kilichopo tandika Dar es salaam Bi, Latifa Masasi wa pili   mpima mtoto Nuru Edward wa kituo cha kulea watoto yatima cha Valentine children home kilichopo yombo buza kulia ni mtoto Clara Olimpia nae akihudumiwa na nesi Mary Hongoli


Muhudumu wa afya ya baba mama na mtoto wa kituo cha alafa kilichopo tandika Dar es salaam Bi, Latifa Masasi wa pili akimpima afya mtoto Lovenes Masawe kulia ni nesi Mary Hongoli

watoto waliojitokezwa kuletwa kwa ajili ya kupima afya na wazazi wao wakiwa katika foleni ambapo jumla ya watoto waliojitokeza ni 230 ambao waliudumiwa na kupewa ushauli wa bule

Saturday, October 10, 2015

Aunt Ezekiel: Stukeni, hakuna mabadiliko bila kufanya kazi


 Na mwandishi Wetu
Watanzania hasa vijana wameshauriwa kuyafikiria kwa umakini mabadiliko wanayoyataka kabla ya kuchukua maamuzi wanaytaka kuchukua, hali itakayopelekea kuwa na umakini watakapofikia siku ya kupiga kura, siku ambayo wanapaswa kufanya maamuzi yaliyp sahihi.

Hayo yamesemwa na msanii wa filamu Aunt Ezekiel ambaye yupo katika kundi la kampeni la Nimestuka linalomuunga mkono mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi, Dk John Pombe Magufuli, ambalo linafanya ziara za kijiji kwa kijiji kuwahamasisha vijana kukipigia kura Chama cha Mapinduzi ili kirudi madarakani kuendelea na utekelezwaji wa ilani yake ya uchaguzi.

Aunt amewaambia wakazi wa Malunga, Shinyanga, wasidanganywe na bei za bidhaa kwamba zimepanda sana ukilinganisha na miaka kumi iliyopita. Hizi bei pia zisingeweza kuwa zile zile kwa miaka kumi, hata wao wangekuwa wafanyabiashara wangepandisha tu.

"Mabadiliko bila na wewe kama kijana kujishughulisha hayawezi kuja, itakuwa ni miujiza, na hii ndio sababu yangu ya msingi nikaamua kurudi kwenye chama cha Mapinduzi ambako mgombea wake anasisitiza vijana kufanya kazi", alifafanua Aunt Ezekiel.

Aunt ambaye alikuwa ni mmojawapo kati ya wasanii wanaoliunga mkono kundi la vyama vya siasa la UKAWA, ame3waambia vijana wa Malunda kwamba vyama vya upinzani, bado havijawa tayari kutawala kwa kuwa linatumia vibaya nguvukazi ya vijana.

"Kule tunafundishwa kulalamika tu, kupinga serikali, hatuambiwi tufanye nini maisha yetu yawe bora, hatuambiwi kuhusiana na kuanzishiwa miradi, hii sio busara hata kidogo
 StanBakora, mmoja kati ya wasanii walio katika ziara ya Kijiji kwa Kijiji ya Nimes'tuka, akiongea mbele ya hadhara Shiyanga mjini
 Mboto naye akimwaga Pipi kwa wakazi wa Malunga
 Miss Tanzania Lilian Kamanzima, naye pia alitoa ujumbe wake 
 Umati wa wananchi wa Shinyanga mjini waliojitokeza katika mkutano wa kundi la Nimestuka uliofanyika katika kata ya Malunga

 Kitale akiingia uwanjani kwa ajili ya kuongea na wananchi wa Malunga...
Inspekta Haroun, ..Babu