Sunday, May 12, 2013

KUMBUKUMBU YA BOB MARLEY ' BOB MARLE DAY' NDANI VIWANJA VYA POSTA

RUGE AOMBA KUKUTANISHWA NA JAY DEE


MKURUGENZI wa Kampuni ya Clouds Media Group, Ruge Mutahaba amesema yu tayari kukutana na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Amos Makalla aliyejitolea kuleta suluhu kati yake na nyota wa kike wa Bongo Fleva, Judith Wambura 'Lady Jaydee', limeandika gazeti la Mtanzania.
Mutahaba ametoa kauli hiyo ikiwa ni siku chache tangu Waziri Makalla atamke kuwa yu tayari kuingilia kati mvutano uliopo baina ya msanii huyo na Ruge kwa kuwaita kuzungumza nao kwa maslahi ya wahusika na tasnia ya muziki nchini.“Mimi kana nilivyosema katika tamko langu wiki iliyopita, kwamba niko tayari tuitwe na watu watusikilize pande zote mbili, hasa mlalamikaji na ukweli uweze kuwa wazi zaidi kwa sababu hadi sasa Lady Jaydee amezungumza mengi,” alisema.
Wakati huohuo, Ruge ameongeza kwamba tayari ameshachukua taratibu za kisheria ikiwa ni pamoja na kufungua jalada polisi la malalamiko ya kutukanwa na Lady Jaydee.“Lakini ninaweza kusema jambo hili linaweza kuzungumzika nje ya vyombo vya sheria kwani sisi tunaliona ni dogo na la mzaha, lakini lina athari kubwa katika jamii inayotuzunguka,” anasema Ruge.Mwanzoni mwa mwezi huu, Lady Jaydee aliamua kuibuka na kuituhumu Clouds Media Group kwa kutumia mitandao ya kijamii kama facebook, twitter na blog yake kuwa inamuhujumu kimuziki, kuzuia matangazo ya mgahawa wake wa Nyumbani Lounge na kipaji chake kwa ujumla, tuhuma ambazo Ruge na Clouds wanazikanusha vikali.


Monday, May 6, 2013

JANUARY MAKAMBA AWAPONDA CLOUDS KWA KUTOPIGA BONGO FLEVA

Huenda mjadala kuhusu uamuzi wa kituo cha radio cha Clouds FM, leo kutopiga Bongo Flava siku nzima haujalikuna sikio la naibu waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba.
Kupitia Twitter, Makamba ameandika kuwa Tanzania ina matatizo matatizo mengi ya kujadili kuliko nyimbo za kuchagua kucheza redioni. “We’ve got much bigger problems than radio playlists, ” ametweet.
Katika mahojiano maalum leo kwenye kipindi cha Power Breakfast cha Clouds FM, mmoja wa wakurugenzi wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba alidai kuwa ametoa amri leo kituo chake kisicheze Bongo Flava.
Uamuzi huo leo umekuwa gumzo kwenye mitandao ya kijamii.

RUGE AMJIBU JIDE KUPITIA POWER BREAKFAST LEO.

Sikiliza alichokisema ruge leo asubuhi.

Friday, May 3, 2013

GADNER ALONGA JUU YA BIFU LA JAYDEE NA RUGE / KUSAGA (CLOUDS)

Kutokana na bifu linaloendelea kati ya msanii Lady Jay Dee na Radio ya Clouds fm, Gadna G Habash ambaye ni Meneja na Mume wa Mwanamuziki huyo maarufu ameibuka na kuzungumzia yale yanayofahamika kuwa  ni wosia wa msanii huyo.
Kupitia kipindi cha The Takeover kinachorushwa na kituo cha TBC fm haya ndio yaliyokuwa majibu ya maswali aliyoulizwa na presenter wa kipindi hicho.

  
Ipi ni Kauli yako juu ya Wosia wa Lady Jay Dee...?
Gadna G: Ni maneno  ambayo yametoka moyoni mwake na  ni maneno  mbayo anajitetea kama msanii,  mimi kama Meneja ukiacha pia kama  mke wangu naendelea kumsapot kwa kile ambacho anaona ni sawa, basi mimi nitaendelea kumsaport  na kujaribu kuzungumza na Lady Jay Dee, mara nyingi anasema tu kwamba  watu wasifikilie ni swala la wimbo kupigwa au kutokupigwa, hayo ni mambo ya kawaida lakini wafikirie tu kwamba huyu mtu anaongea kutokana experience yake aliyokuwa nayo na wale watu.

Baada ya mwaka 2003 kuacha kufanya kazi kwenye management yao ya Smooth Vibe, yalitokea mambo mengi hapa katikati  ila hakusema lakini siku za hivi siku za karibuni kuna mengine ambayo yametokea, ndio akaona hapana nisipo sema nitazidi kukandamizwa na matokeo yake nitakufa kisabuni.

Hii ni kama vita mmejipangaje..?
Gadna G: Unapoamua kusema ukweli swala la kujipanga mara mbili huwa halipo, ni kwamba unasema ukweli watu wasikie  naukizungumzia uhasama watu watauliza juu ya uhasama  lakini ulikuwepo tayari kwahiyo tu watu wanajua kwa sasa kwa kuwa jdee ameamuwa kuongea lakini tu hawajui tu kwamba jdee alikuwa na matatizo na wale watu tangu kipindi cha nyuma sababu wale watu wanafumo dume ya kufanya kazi na alipoachananao aliona kama wanamfatilia  kulekule ambapo yeye alipo

Nini mlikiona kama chokochoko...?
Gadna G
: Unajua kwa mfano unaweza kumuomba mtu maji akakwambia sina, ukayaona yale  pale ukamwambia niuzie akakuuzia ila bado alivyokuuzia  akaona kama unafaidi, mwisho  akakwambia yameisha nenda sehemu nyingine, ukaenda sehemu nyingine na ukayapata bure, akaona umepata akaamua kukufata kulekule na akakukuta unakunywa maji kwenye grasi kisha akakuputa, sasa hapo inabidi useme hapa unavyofanya sio sawa ndo hicho anachofanya Jay Dee sasa hivi.

Hali hii imewaathiri kwa kiasi gani...?
Gadna G:
 Cha kushukuru Mungu ni  kwamba msanii au hata pia stesheni ya redio inategemea umma wa Watanzania au  hata mashabiki kwa ujumla kwa kuwepo kwake.

Jay Dee anapata saport nzuri kutoka kwa Watanzania, basi ujue hata hajaathirika chochote, na pia tu anaendelea kufanya kazi kwa bidii, ila tu isipokuwa unapoona mtu anafanya madhara ili tu mtu apate athari fulani ndio unasimama kuongea, ndiyo maana tuna Bunge na watu wanasimama, watu wanaongea, watu wanatetea hoja, ndiyo maana yake.

 Yani lazima mtu usimame useme ukweli kwa unalohisi hili jambo litanipa madhara nisiposema.

Kwa Wasanii wengine unawaambiaje...?Gadna G: Uwoga ni kitu ambacho binadamu tumeumbiwa, wakati mwingine unasaidia wakati mwingine unakudhiru uwoga wako,kwa sababu wanasema adui wa maendeleo yako mwenyewe ni wewe mwenyewe, ndiyo maana uwoga wako unaeza ukasabishwa ukakandamizwa zaidi, ndiyo maana wazee wetu waliweza kusimama na kuikomboa hii nchi kwa sababu walisimama hawakuogopa. 

Wangeogopa hii leo hii nchi tusingekuwa huru, kwa hiyo kama kuna mtu ana jambo na anaogopa kusema hilo ni jambo la kawaida kuogopa, lakini wakati wa kusema ukifika usiogope kusema ili mradi useme ukweli, basi inatosha....

Kauli yako ya mwisho ni ipi..?
Gadna G:
 Ni kwamba wanahitaji kujua ukweli na kuambiwa ukweli, mtu yoyote anayejua kitu cha kweli  anaweza kusema sio sawa, utaendelea kukandamizwa. Kauli ya mwisho  ndo hiyo wanahitaji kuambiwa ukweli na  kusikia ukweli  ili kama wanakosea wasiendelee kukosea  wabadilikee….

Wednesday, May 1, 2013

JAMBO SQUAD - TUKUNYEMA (OFFICIAL VIDEO)

JAY DEE: HUU NI WOSIA WANGU KAMA IKITOKEA NIMETANGULIA KUFA KABLA YA RUGE AU JOE KUSAGA

Watu wanashtuka mtu akiongelea kifo, Utafikiri hawafahamu fika kuwa kila nafsi itakionja, Kwenye maisha yangu nimepitia mambo mengi, magumu na mepesi
Na bado naendelea ku experience mambo magumu zaidi kadri ninavyozidi kuwa mkubwa.
Siku za karibuni nimekuwa nikipigwa vita sana na watu wenye uwezo mkubwa kifedha , ki umri na hata wenye ukubwa wa connection katika hii industry ya muziki. Wanaomiliki chombo cha habari.
Nasimama na kusema kuwa sitokata tamaa, kwani lengo lao kubwa ni kuona na kuhakikisha nimeanguka kabisa na sipo katika ramani ya muziki.
Watu hao ambao vita yao ilikuwa baridi miaka kumi iliopita, sasa inazidi kuwa moto baada ya kutambua kuwa mimi ni mtu mwenye maamuzi yangu na misimamo yangu bila kuburuzwa.
Wanapita kila mahali kuhakikisha kila mrija unaoniingizia chochote unakatika, na hiyo ni kutaka kuuthibitishia umma wa Tanzania kuwa hakuna msanii anaeweza ku survive bila wao.
Mimi ni msanii tofauti na hao mnaofikiria.
Nadhani mnafahamu tangu niachane na Tuzo zenu mnazo influence nani apate nani asipate, na tangu niachane na Fiesta nilipolipwa laki 8 mara ya mwisho na kuamua kuunda Band ili nijiajiri na kupata shows zangu mwenyewe, ikafanikiwa sana jambo ambalo limewauma na kuamua kufanya kitu cha kuiangusha Band yangu.
Nita survive kwa njia zozote MUNGU alizonipangia.
Wakati bado wote tunapumua na kwakuwa watu hao hawanipendi kabisa, Naamini fika hawataweza kunipenda hata siku nitakapokuwa nimekufa.
Na huu ndio wosia wangu kwa watu hao.
Natambua wanaweza kutumia redio yao kutangaza sana kifo changu na kusema marehemu alikuwa mtu mzuri na pengine kupiga nyimbo zangu kuanzia asubuhi mpaka jioni.
Ila naomba nitamke hivi, siku nikifa CLOUDS FM isipige nyimbo zangu, wala isiongelee lolote kuhusiana na kifo changu.
Ruge Mutahaba na Joseph Kusaga wasihudhurie msiba wangu, na mkiwaona muwapige mawe Enyi mtakaokuwa hai baada yangu.
Kama wamenifitini, na hawajanipenda nikiwa hai Hakuna haja ya kujifanya kunipenda nikiwa marehemu.
Sina haja wanipende pia kwakuwa mimi sio ndugu yao, Ila ubaya wanaoundeleza mioyoni mwao wanaujua na nina hakika nafsi zao zinawasuta pia.
Niliamua kujiepusha nao miaka mingi na kufanya biashara zangu, nimekaa kimya watu wanafikiri nabebwa lakini sijabebwa chochote sikutaka ugomvi haya mambo yalianza baada ya Album yangu ya pili ya Binti mwaka 2003 nilipojitoa Smooth Vibes chini ya Ruge.
Nilivumilia fitna nikiamini ipo siku yatakwisha lakini naona moto ndio unazidi kuwaka.
Na hii ni kwasababu wanaogopa msanii akiwa mkubwa watashindwa kumuamrisha, Hamuwezi kumiliki dunia..
Kama mnasema mlinibeba mbona hamkuwabeba dada zenu wa tumbo moja waimbe ili hela irudi nyumbani??. kama kweli wewe Kusaga unajua kubeba basi beba jiwe liimbe liwe star..
Kwa roho zenu mbaya mnaweza kumbeba mpita njia nyie??.
Talent haibebwi, hujibeba kama mnabisha si mna watoto wabebeni basi wawe kama kina Diamond ndio nitaamini kweli nyie mnaweza kubeba watu.
Mnawatishia wasanii kuwa yoyote atakaefanya nyimbo na mimi hazitapigwa, vikao vinne mmeshakaa kunijadili.
Mnadhani je! nitapungukiwa nini endapo wasanii wengine wakiacha kufanya kazi na mimi?? nyimbo hazitakuwa nzuri.
Basi sawa ngoja tuone MUNGU ni nani, Binadamu nani??
Kwahiyo mtaamrisha watu pia wasikae na mimi??
Ilikuwa niseme majina matatu huyo mmoja nimemsamehe baada ya kugundua sio hiyari yake ila yuko under influence ya hawa jamaa wawili.
Kila siku mnamsingizia Ruge peke yake Kusaga ni mfitini kuliko hata huyo Ruge, watu hamjui tu.
Mtu hela zote hizo bado shillingi mbili ya Jide inakuuma??
Roho gani hiyo??
Naishia hapo na sitabatilisha kauli yangu

JIDE

Monday, April 29, 2013

EXTRA BONGO YAZIDI KUWABAMBA MASHABIKI NDANI YA MEEDA SINZA JANA USIKU

Mkurugenzi wa Extra bongo Ally Choki akiimba mbele ya mashabiki wake (Hawapo Pichani) ndani ya Ukumbi wa Meeda sinza jana Usiku wakati bendi yake ilipokuwa ikiburudisha pande pande hizo
Kushoto ni mmoja wa marapa bora wa muziki wa dansi Totoo Ze Bingwa akirap ndani ya Meeda sinza wakati Bendi anayopigia mzigo Extra Bongo ilipokuwa ikitumbuiza pande hizo na kulia ni Banza Stone a.k.a Generale akimpa big up.
Rapa bora wa Extra bongo Kabatano (Kulia) akigani moja ya jimbo zao bora huku akipewa sapoti na nguli wa muziki wa dansi Banza Stone mwana masanja wakati bendi hiyo ilipokuwa ikitumbuiza maeneo ya Sinza katika ukumbi wa Meeda jana usiku.
Wakata nyonga maarufu kwa sasa wa Extra bongo wakiongozwa na nyamwela wakiwapagawisha mashabiki waliohudhuria shoo hiyo ndani ya Meeda Sinza jana usiku

MBUNGE WA ARUSHA MJINI, GODBLESS LEMA APANDISHWA KIZIMBANI LEO

Wednesday, April 24, 2013

SHABANI MHAMILA 'STAR BOY' AJIFUA KUMKABLILI JIBABA MEI MOSI


Bondia Shabani Mhamila 'Star Boy' kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Chalo Issa wakati wa mazoezi yanayo endelea katika kambi ya ngumi Ilala Star Boy ana jiandaa na mpambano wake na Yusuph Jibaba uatakaofanyika mei mosi katika ukumbi wa PTA Sabasaba .

Bondia Shabani Mhamila 'Star Boy' kushoto akioneshana uwezo wa kutupiana makonde na Ibrahimu Class 'King Class Mawe' mabondia wote wanajiandaa kwa ajili ya mashindano yatakayofanyika siku ya mei mosi katika ukumbi wa PTA Sabasaba 

Kocha wa mchezo wa masumbwi nchini Habibu Kinyogoli kushoto akimwelekeza jinsi ya kutupa makonde bondia Shabani Mhamila 'Star Boy'  katika kambi ya Ilala iliyopo Amana CCM jana Sta Boy anajiandaa na mpambano wake na Yusuph Jibaba utakaofanyika siku ya mei mosi katika ukumbi wa PTA Sabasaba Dar es salaam.
Picha Zote na www.superdboxingcoach.blogspot.com


Na Mwandishi Wetu
BONDIA Shabani Mhamila 'Star Boy' anaendelea kujifua kwa ajili ya kumkabili Yusuf Jibaba katika ambano la utangulizi wakati wa mchezo wa kati ya Francis Cheka na Thomas Mashali.
Pambono la raundi nne linatarajiwa kufanyika katika Ukumbi wa PTA Sabasaba, Dar es Salaam Mei Mosi mwaka huu, linatarajiwa kuwa la vuta
nikuvute kutokana na kila mmoja kujigamba kujiandaa vema.
Kocha wa Star Boy, Habibu Kinyogoli 'Masta' akisaidiwa na  Rajabu Mhamila 'Super D' wamesema kuwa
bondia wao anaendelea vizuri na mazoezi kwa ajili ya  kujiandaa kumchakaza Jibaba ili
kuendelea kujiwekea sifa nzuri.
"Bondia wangu yuko katika maandalizi ya kutosha kuhakikisha anafanya
vizuri katika pambano hilo la utangulizi kati ya Cheka na  Mashali" alisema
Super D na kuongeza Star Boy alishawai kuwa bingwa wa masumbwi mwaka 1998 ambapo alisimama kwa kipindi kidogo kutokana na maisha ya nchini rakini kwa sasa ameamua kurudi katika ulingo wa masumbwi ili aweze kutoa changamoto za mchezo uho kutokana na mabondia wengi awajui sheria na kanunu za mchezo huo Sta Boy mwenye rekodi ya. won 14 (KO 5) + lost 7 (KO 4) + drawn 2 = 23 ambaye mkanda wa kwanza wa taifa alichukua kwa kumtwanga  Theodor Luanda
Frebruary 2,1996 na kutetea vema 

Thursday, April 18, 2013

BONDIA FADHILI MAJIHA ARUDI NA UBINGWA KUTOKA INDONESIA BAADA YA KUMDUNDA HERI AMOL

Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto akifuraia na bondia pendo Njau baada ya kumpokea bondia Fadhili Majiha (katikati) aliyerudi na kombe la ubingwa aliouchukua Indonesia wiki iliyopita  baada ya kumtwanga bondia Heri amol wa pili ni Japhet Kaseba mwingine ni Kanda Kabongo.

Wednesday, April 17, 2013

HISTORIA FUPI YA MAREHEMU BI KIDUDE (FATMA BINT MBARAKA), KUZIKWA KESHO SHAMBANI KWAO ZANZIBAR

Mwanamuziki mkongwe katika Taarab Fatuma Bint Mbaraka maarufu kwa jina la Bi Kidude aliyefariki dunia leo asubuhi huko Bububu Zanzibar, alikokuwa anaugulia kwa kipindi sasa. 
Mwili wa Bi Kidude utahamishiwa kwake Rahaleo na mazishi yatakuwa kesho. 
Bi Kidude alizaliwa katika kijiji cha Mfagimaringo, alikuwa binti wa mchuuzi wa nazi, hakuna anayejua haswa Bibi huyu alizaliwa tarehe ngapi, kuna hata mawazo kuwa alikwishafikisha miaka 102. 
Katika mwaka 1920 tayari alikuwa amekwisha anza kuimba katika vikundi vya sanaa kule kwao, mwaka 1930 alijiunga na Egyptian Musical Club ya Dar es Salaam na kuzunguka miji mingi ya Tanganyika wakati ule , mwaka 1940 alirudi Zanzibar ambako awali alikuwa amekimbia kwa kuwa aliozwa kwa nguvu na mtu aliyemzidi sana umri.
Bi Kidude pia liwahi kuimba na Sitti Binti Sadi wakati wa ujana wake, na katika maisha yake Bi Kidude amekwisha zunguka mabara yote akiimba katika majukwaa na wanamuziki maarufu ulimwenguni

BI KIDUDE KUZIKWA KESHO SHAMBANI KWAO ZANZIBAR
Bi Kidude anatatarajiwa kuzikwa kesho huko Zanzibar.

SULE'S INC & ENTERTAINMENT na Timu nzima ya Blog ya MTOTO WA KITAA ina toa pole kwa fwamilia, ndugu jamaa na marfiki na TAIFA kwa kufikwa na msiba huu
Mungu Amlaze Pema Peponi Bibi yetu. Amen

MKONGWE WA MUZIKI WA TAARABU NCHINI, BI KIDUDE AMEFARIKI DUNIA.


Bi Kidude katika moja ya shoo zake enzi ya uhai wake
*********************

Bi.Kidude amefariki dunia mjini Zanzibar. Bi Kidude alikua akisumbuliwa na ugonjwa wa Kisukari Habari zaidi tutaendelea kuwaletea kile kinachoendelea.

Monday, April 15, 2013

MSARABA MWEKUNDU TAWI LA KISUTU WAPATA MSAADA WA VITI VYA WANAFUNZI


Meneja Masoko wa Kampuni ya Palray watengenezaji wa fenicha mbalimbali, Thomas Simpokolwe kulia akimkabidhi mwanafunzi wa chama cha msaraba mwekundu tawi la kisutu, Grace Raphael sehemu ya msaada wa viti kwa ajili ya kusoma masomo mbalimbali ya uokoaji kulia ni Mwenyekiti wa msalaba mwekundu tawi la kisutu Bw.Rashid Mkawa


Wanafunzi wa Msaraba Mwekundu Tawi la kisutu wakisaidiana kubeba madawati waliyo kabidhiwa
picha na www.burudan.blogspot.com

NEW SONG FROM JCB FT CHABA & BEN POL - I DONT CARE


HEKAHEKA MITAA YA KATI: JAMAA APOKEA KICHAPO BAADA YA KUSHINDWA KUMLIPA CHANGUDOA


Neema Samson (Changudoa) akiwa amemkaba mteja wake baada ya kushindwa kumlipa chake.

Joseph akizidi kupewa hali ngumu na Neema, pembeni wananchi wakianza kusogea eneo la tukio.

 Baada ya wananchi waliingilia kati zogo hilo baada ya kuona wanazidi kuvuruga amani mtaani kwao, waliamua kuwaweka mtu kati tayari kuwapeleka sehemu husika.

Wananchi waliamua kuwapandisha kwenye Bajaj tayari kuelekea kituo cha polisi.

Sunday, April 14, 2013

BREAKING NEWS!!!!!!!! ......SHULE YA SEKONDARI YA WAZO HILL INAENDELEA KUUNGUA

Tarfa zilizotufiki muda huu ni kwamba shule ya Sekondari ya Wazo Hill ya jijini Dar es Salaam inaendelea kuteketa kwa moto huku juhudi za kuuzima moto huo zikiendelea kufanyika.
......Wanahari wa Blog hii wapo njiani kuelekea katika eneo latukio.
...Tutaendelea kuwaletea kile kilichojiri.

Saturday, April 13, 2013

MTANDAO WA PR HABARI WAPATA MKOKO WAKE


Mwenyekiti wa  Mtandao wa kijamii wa http://prhabari.blogspot.com/, Spear Patrick akiwa amepozi na gari hilo

GARI HIYO INAVYO ONEKANA KWA NYUMA