b..

B1

Wynem

animation

Sunday, August 20, 2017

BONDIA SELEMANI SIMBA HAPANIA KUTOA KICHAPO KWA MABONDIA KUANZIA AGOST 26 VIJANA


Na Mwandishi Wetu
BONDIA wa ngumi za kulipwa kutoka Singida Selemani Simba 'Singida Unaited' amendelea na mazoezi ya kujifua kwa ajili ya mpambano wake wa Agost 26 utakaofanyika katika ukumbi wa Vijana Kinondoni ambapo atapambana na Kallage Ramadhani bondia anaenolewa na kocha mkongwe katika ngumi Rajabu Mkamba

Akizungumzia mpambano wake Simba amesema kuwa amekuja Dar kwa ajiri ya kupambana na kuwapiga mabondia wote watakaopambana nae wakati wowote ule bondia huyo mpaka sasa kashapigana mapambano mawili kati ya hayo mawili kashinda moja na kudundwa moja

akizungumzia matarajio yake katika masumbwi amesema anatamani kufika mbali zaidi kama Ibrahimu Class 'King Class Mawe' walivyofanikiwa kufika mbali na mpaka sasa kuwa bingwa wa Dunia

katika mpamano uho siku hiyo kutakuwa na mapambano mengine ya ubingwa kati ya bondia Fransic Miyeyusho 'Chichi Mawe'  na Baina Mazola 'Simba Mazola'
mapambano mengine ya siku hiyo ni sajo bosco Jr atakumbana na juma rashidi mdobi na Issa Nampepecha ataoneshana umwamba na Abbas Mwamba wakati Karim Ramadhani ataoneshana kazi na Yohana Dhobian na Keisii Amali atakuchiana ngumi na Hashimu Chisola na Said Wigo atazipiga na Chicho Ramadhani

Mapambano haya yote yatasimamiwa na Kamisheni ya ngumi za kulipwa nchini TPBC ambayo yenye dhamana ya kuendesha mchezo wa ndondi za kulipwa nchini

Katika mpambano huo siku hiyo kutakuwa na uzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi  kali pamoja na kutambua sheria zake zikiwa na mabondia wakali kama vile:-

Manny Paquaio, Saul 'canelo' alverez, Floyd Mayweathar,Mike Tyson,Mohamed Ali,Ferex Trinidad, Miguel Cotto na wengine wengi
pia kuta kuwa na vifaa vya mchezo vitakaokuwa vikitolewa na Rajabu Mhamila 'Super D' kwa mabondia watakaofanya vizuri siku hiyo na vingine kuuzwa kwa pesa taslimu na kocha huyo kwa ajili ya kuhamasisha mchezo wa masumbwi

No comments:

Post a Comment