b..

B1

Wynem

animation

Thursday, April 24, 2014

BANZA STONE, CHOKI KUUNGURUMA NDANI YA RUFIT KESHO (IJUMAA 25/04/14)

Wakali wa muziki wa dansi bongo, mtu mzima Ally Choki na Banza Stone kwa pamoja watadondosha bonge la Shoo pande za Tabata katika ukumbi wa Rufita Executive ikiwa na shoo iliyondaliwa maalumu na Kampuni ya BS ENTERTAINMENT .
Akizungumza na mwandihi wetu Banza Alisema kuwa wamejipanga vya kutosha kuwapa raha na burudani ya kutosha mashabiki wao wote na wakazi wa maeneo ya tabata Segerea siku ya Ijumaa ya tarehe 25 mwezi wa nne.
"kiukweli mashabiki wetu wajitokeze kwa wingi maana tumeamua kuwapa burudani ya kutosha nikiwa na bendi nzima ya Extra Bongo na mtu mzima Ali Choki"
kwa kuongezea Banza alisema kuwa amewaandalia mashabiki wake vitu vizuri ambavyo hawajawahi kuvipata kwani watawaimbia nyimbo ambazo ni mpya zikiwamo zile walizoimba na marehemu mzee Gurumo. "Kuna nyimbo nyingi tutaanza kuziimba pale ikiwa ni pamoja na zile tulizoimba na mzee wetu marehemu Muhidini Gurumo ikiwa ni 'Surprise' kwa mashabiki wetu wa maeneo ya Tabata Segerea"
Banza alimalizi kwa kushukuru uongozi wa Kampuni ya BS ENTERTAINMENT kwa kuwaandalia shoo hiyo itakayotoa burudani ya kufa mtu huku akitaja kiingilio katika shoo hiyo ni Sh. 5000/= tu malngoni.

Wednesday, April 23, 2014

JACKLIN WOLPER, LULU WAKIRI KULA URODA NA ALIKIBA

Ali kiba ni mmoja wa wanamuziki walio kimya sana kwenye upande wa kuongelea mambo yake binafsi, haswa kimahusiano, au hata kujitangaza kumiliki kitu kingine chochote cha thamani kama ilivyo desturi ya wasanii wengi hapa town baada tu ya kupata umaarufu, ila siri hufichuka haswa pale kwa warembo hawa wanapoamua kumwaga mpunga ndipo hapo unapoanza kujua yaliyo chini ya kapeti.Hawa ni warembo waliowahi kukiri kuwa walishawahi kuwa na mahusiano na Celeb huyu mkongwe sana kwenye anga za muziki huu wa Bongo Fleva.
 
Lulu na Kiba.
Haikujulikana mapema kama inavyotokea kwa watu maarufu wengi hapa town, ila mahusiano yao yalianza huko kitabo sana, baina ya Lulu na Ali Kiba, ila mwisho wa siku Lulu aliamua kumwaga mpunga hadharani kufunguka juu ya mahusiano yao.
“Duh! Umenikumbusha mbali sana. Nilishasahau kabisa kama niliwahi kutoka naye. Pamoja na kwamba ni kweli alikuwa mtu wangu, lakini kwa sasa moyo wangu hautaki kusikia kingine zaidi ya Bieber na namuonea wivu sana Selena Gomez (mpenzi wa Bieber).”
ila hakutaka kuzungumzia sababu za kuachana naye, nakusea ilikuwa tu sababu zake binafsi kwa sababu mapenzi yana taba moja kuwa ukiyag’ngania hasa pale ambapo hauenjoy mwisho wake ni kuumizana tu, alimalizia lulu kuelezea safari yake ya mapenzi, na hadi hivi sasa anakiri kuwa bado yupo yupo sana.
  
Wolper na Kiba.
Mapenzi ya hawa wawili inasemekana yalianza enzi hizo ambapo wawili hao walikuwa bado hawana majina kabisa hapa town, kila mmoja wao akiwa yupo kwenye hustle zakutoka kila mmoja akiwa natetea fani yake, ila kwa bahati nzuri AliKiba akaanza kupata umaarufu kuitia muziki hata kabla ya Wolper kuanza ku-make headlines kupitia filamu, akiwa kama muigizaji.
“Ni kitambo kidogo sana wote hatukuwa star lakini mwenzangu alifanikiwa kuchomoka,lakini Ali ndiye aliyeniingiza kwenye ulimwengu wa Mapenzi” alifunguka Wolper,
“Ali akawa star,alipokwenda nje nikasikia wanawake wanamshobokea,sasa mimi sikutaka karaha nikakaa pembeni,lakini jamaa ni mtu poa sana na tukikutana tuanasalimiana freshi kabisa” alimalizia akizungumzia sababu zilizomfanya aachane na Kiba wakati huo.

Sunday, April 13, 2014

HII KALI!! HAWA NDIYO WANAMUZIKI WA KIUME AMBAO MPAKA LEO WANAISHI KWA MAMA ZAO (WATOTO WA MAMA)

Chid Benz
Anaishi kwa maam yake, Ilala pale maflat ghorofa ya juu kabisa
Jux
huyu pia anatumia zaidi mpunga wa mama kufanyia promo ya nyimbo zake still njemba inaminya home japo yupo china ila akirudi movie linaendea kwa mama jux
GosBy
huyu jank kwa mama ndio kila kitu anaitwa agripina
Dullayo
nyumbani ni majumba sita na hakuna mipango ya kutoka hapo born home die home

Chanzo ni HAPA

Wednesday, April 2, 2014

HIZI NDIO PICHA ZA KINA KOLO NA MUSTAPHA ZILISABABISHA MSANII NYOTA NDOGO KUANDAMANA

Screen Shot 2014-03-25 at 1.29.26 AM
Colonel Mustapha ni miongoni mwa Wasanii wa longtime kidogo kwenye game ya muziki Kenya toka enzi hizo akiwa kwenye kundi lililotoa hit single yenye maneno ‘bibi yake mufupi, kijana murefu ametoka wapi’
Hivi karibuni ameingia kwenye vichwa vya habari sana hasa baada ya kutangaza kuwa mapenzini na Huddah, mrembo aliewahi kuiwakilisha Kenya kwenye shindano la Big brother Africa ambapo uhusiano wao hauchukua muda mrefu ukavunjika.
Kabla ya kuvunjika, tayari walikua wameshapiga picha ambapo Mustapha anasema alikua amerekodi wimbo na Huddah lakini walipoachana mrembo huyu akasema Ogopa Dj’s wasiitumie tena sauti yake kwenye huo wimbo na kama watafanya hivyo atawashitaki.
Hata hivyo picha zao wawili zilishasambaa kwenye internet tayari na kuanza kuchukua headlines kutokana na pozi zao.

Screen Shot 2014-03-25 at 1.29.51 AM
Kuonyesha kupinga hiki kitendo, mwimbaji staa wa ‘watu na viatu’ Nyota ndogo aliungana na Wanawake wengine Mombasa na kuandamana kupinga kitendo cha Mustapha kuzisambaza picha zinazomdhalilisha Mwanamke hivyo aombe msamaha haraka iwezekanavyo.
Screen Shot 2014-03-25 at 1.30.18 AM
Namkariri Nyota akisema ‘Mustapha ambae ni msanii mkubwa ameanza muziki kitambo kuchukua picha za watoto wa kike na kuwavua nguo, hii itanyima hata Wazazi kuachia watoto wao kufanya muziki unaoonekana uhuni… ikiwa Mustapha hatoacha hii itatuharibia, kama kaona ameshindwa kutunga nyimbo zitazowashika watoto wa sasa hivi afate mtoto amuandikie’
‘Ameona jina linashuka ndio maana bora achukue picha za uchi atengeneze skendo, Mustapha nimekua nae kwenye muziki miaka mingi, kwa nini sasa hivi ndio afanye kwa sababu Prezzo anafanya? ama ameona Prezzo yuko juu kwa sababu anafanya.. yeye ndio anatakiwa kumwambia Prezzo usifanye hivi’

Screen Shot 2014-03-25 at 1.34.45 AMScreen Shot 2014-03-25 at 1.35.12 AM
Hata hivyo Mustapha amezungumza baada ya haya maandamano na kusema ‘Ni kitu cha kushtua kuona maandamano yamefanyika kwa ajili ya Mustapha, wakati tunapiga hizi picha hakukua na lengo lolote la kumdhalilisha Mwanamke bali ilikua mambo yetu yenyewe kwa raha zetu, nilivyoona youtube kuhusu haya maandamano nimehuzunika… naomba msamaha kwa yeyote aliekerwa na hili… nimekubali kuomba msamaha kwa Wanawake’
Kwa kumalizia Mustapha amesema ‘kuna Wasichana ambao wanataka tupige hizo picha na wananilipa’

Screen Shot 2014-03-25 at 1.37.19 AM