b..

B1

Wynem

animation

Monday, March 28, 2011

20% AFUNGUKA NA KUSEMA MANI WALTER ALISTAHILI TUZO.


     http://1.bp.blogspot.com/-n1aU-6YDUOg/TZBLi-eDwzI/AAAAAAAADOI/pexPCqHZOQM/s1600/20%2Bpercent.JPG
Baada ya kushinda tuzo 5 za Kili Music Awards 2010/2011 na kuweka historia,amefunguka kuwa hakutegemea kama angeshinda tuzo zote 5 kwenye vipengele ambayo ameshiriki!  
"Sikutegemea kama ningepata tuzo hizo zote 5 kwani nilitegemea tuzo 2 kiuhakika....ya wimbo Bora wa Afro Pop na Mtunzi Bora wa Nyimbo,ila kushinda tuzo ya Msanii Bora wa Kiume,Muimbaji Bora wa Kiume na Wimbo Bora wa Mwaka - Tamaa Mbaya,kiukweli sikutegemea kabisa" 
Kuhusu Producer wake Man Water wa Combination Sound aka Combinenga kutopata tuzo ya Mtayarishaji/Producer Bora wa Muziki-2010,20% amesema kuwa Man Water alistahili coz kama yeye amepata tuzo zote 5 kupitia nyimbo ambazo Man Water amezitengeneza za Malumbano na Tamaa Mbaya,lakini tuzo imeenda kwa Producer Lamar toka FishCrab Studio haiko sawa kabisa...alifunguka 20% akiwa njiani kurejea Dar na akiwa kwenye basi akirudi,nyimbo zake ndio zilikua zinapigwa njia nzima bila hata ya kuwaambia wenye basi

20% amechukua tuzo hizo kupitia vipendele vifuatavyo;
1.Tuzo ya Mtunzi Bora wa nyimbo - 2010
2.Tuzo ya Wimbo Bora wa Afro Pop - Tamaa Mbaya
3.Tuzo ya Mwimbaji Bora wa Kiume - 2010
4.Tuzo ya Wimbo Bora wa Mwaka 2010 - Tamaa Mbaya
5. Tuzo ya Msanii Bora wa Muziki wa Kiume - 2010

No comments:

Post a Comment