b..

B1

Wynem

animation

Friday, August 27, 2010

WASHIRIKI WA VODACOM MISS TANZANIA WAKIWA MONDULI MKOANI MANYARA.

Paulina Lowasa dada wa Mbunge wa Monduli na Waziri Mkuu wa Zamani, Edward Lowasa, akiwapa mkono wa kuwatakia heri Warembo wa Vodacom Miss Tanzania alipokutana nao Wilayani Monduli mkoni Arusha jana na kuwapa zawadi ya vikoi vya kimaasai warembo wote 30. Warembo hao wanatembelea Kanda ya Kaskazini kuangalia vivutio vya Utalii nchini.

  
Baadhi ya Warembo wa Vodacom Miss Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Wasichana Maasai iliyopo Monduli Mkoani Arusha wakati wa rembo hao walipotembelea shule hiyo jana wakiwa katika ziara yao ya kutembelea vivutio vya utalii na kuhamasisha utalii wa ndani nchini.

  
Mkurugenzi wa Lino Interanational Agency, Waandaaji wa Vodacom Miss Tanzania 2010, Hashim Lundenga akizungumza na wanafunzi wa Shule ya sekondari ya wasicahana Maasai ya Mkoani Arusha jana wakati warembo wa Vodacom Miss Tanzania walipoitembelea shule hiyo na kuzungumza na wanafunzi.

  
Baadhi ya warembo wa Vodacom Miss Tanzania 2010 wakimkabidhi chandarua Mria Charles, mmoja wa wagonjwa katika Hospitali ya Mto wa Mbu Mkoani Manyara jana wakati warembo hao walipombatana na Balozi wa Kampeni ya Malaria Haikubaliki Mwasiti Almas (watatu kulia). Warembo wa Miss Tanzania wapo Kanda ya Kaskazini kutembelea vivutio vya utalii na kuhamasisha utalii wa ndani nchini.

 
Mshiriki wa Shindano la Vodacom Miss Tanzania 2010,akigawa chandarua kwa mmoja wa wakazi wa Mto wa Mbu Mkoani Manyara jana katika utekelezaji wa Kapeni ya malaria. Warembo hao wapo Kanda ya Kaskazini kutembelea vivutuio vya Utalii na kuhamasisha Utalii wa Ndani Nchini.

No comments:

Post a Comment