b..

B1

Wynem

animation

Thursday, August 19, 2010

WALIMBWENDE WA VODACOM MISS TANZANIA KUANZA ZIARA LEO

Mkurugenzi wa Miss Tanzania bw. Hashimu lundenga akimtambulisha Mlezi wa kambi mbi ya Vodacom miss Tanzania



Mlezi akionge na warembo pamoja na waandishi wa habari mara baada ya kutambulishwa na kukaribishwa Wanaofuatia katika picha ni Hashim Lundenga Mkurugenzi Miss Tanzania, Bosco Majaliwa Katibu Mkuu Miss Tanzania na Charles Bekon Mkurugenzi wa Giraffe Ocean View Hotel.


warembo wakisikiliza kile wanachoambiwa na mlezi wao huku wakipgwa picha mbili tatu na waandishi pamoja na wapiga pcha.

 

Kaka mkubwa John bukuku kutoka blog ya fullshangwe akipata msosi baada ya kazi nzito ya kuwapiga picha walimbwende. 

Warembo wakipata chakula cha mchana kwa pamoja


Warembo wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kutoka kwenye utambulisho wa mlezi wao.


Walimbwende wanawania taji la Vodacom Miss Tanzanialeo wamesafiri ka ajili ya kuanza ziara mikoa ya kaskazini ambapo wataweka kambi mjini Moshi na hatimaye Arusha na baadae Tanga.
Hayo yalisemwa na meneja mawasiliano wa vodacom bi Nector Pendaeli Foya jana katika pale Hoteli ya Girafe ambapo ndipo kambi ya miss Tanzania ilipo. “mamiss wetu wataondoka kesho kwenda moshi na arusha ambapo warembo watafanya shughuli za kijamii, na huko watakaa kwa muda wa wiki moja” alisema Nector Foye.

Pia mkurugenzi wa Miss Tanzania bw. Hashimu Lundenga alitumia muda huo kumtambulisha kwa warembo na waandishi wa habari ndg. Emanuel Olemaiko kama ndio atakae kuwa mlezi wa kambi ya Vodacom Miss Tanzania

Akiongea mara baada ya kukaribishwa na kutambulishwa Ndg. Ole Naiko aliwaasa walimbwende hao wapendane na waishi kwa kushikiana wakiwa kambini nahata pale anapotangazw mshindi basi wasio shinda wasikasirike kwa maana katika mashindano ni lazima apatikane mshindi, pia Olemaiko aliishauri kamati ya Miss Tanzania kuendeleza shughuli za kijamii kupitia mshindi wa Miss Tanzania.

Ole Naiko amesema anafurahishwa sana na mkataba uliosainiwa na pande mbili zote Kamati ya Miss Tanzania na warembo washiriki wa shindano hilo na ameongeza kuwa warembo hao watangaze vyema utalii wa Tanzania kwani mrembo wa Vodacom Miss Tanzania ndiyo kioo cha Tanzania katika fani hiyo na kielelezo cha nchi kwa hiyo ni vyema wakawa na tabia njema.


No comments:

Post a Comment