b..

B1

Wynem

animation

Friday, August 27, 2010

FRANCIS CHEKA KUCHEZA FILAMU YA HISTORIA YA MAISHA YAKE!!






 BINGWA wa masumbwi Tanzania Francis Cheka anatalajia kuonekana duniani kote kupitia filamu maalum itakayohusu historia ya maisha yake tokea utoto mpaka mafanikio katika mchezo huo hapa nchini

.
Akiongea na waandishi wa habara jijini Dar es Salaam, mtayalishaji wa filamu hiyo hapa nchini kupitia kampuni ya Real Peoples Enterprises (RPE) Amon Ntevi alisema kampuni yake ipo katika hatua ya mwisho kupiga picha maeneo mbalimbali ikiwa ni sambamba na kuingiza matukio aliyofanya ndani nje ya Tanzania kwenye masumbwi.
“Filamu hii itakua ya pekee na ya kwanza kutengenezwa kwa hapa nchini ambapo itaonyesha uhalisia wa bondia Cheka tokea alipokua kijana mdogo na maisha aliyopitia hadi mafanikio katika mchezoo wa ngumi hapa nchini’ alisema Amon.
Pia alisema kuwa watanzania na washabiki wake duniani kote watapata kumjua kwa undani kupitia filamu hiyo itakayojaa simulizi na vitendo kutoka kwa Cheka mwenyewe.
“Wengi wanamuona Cheka kama bondia lakini hawajamjua kwa undani zaidi hivyo kupitia filamu hiyo wataweza kumjua kwa undani ni pamoja na kuingiza matukio ambayo washabiki hawakuwai kuyaona.
Kampuni ya RPE, inayojishuhurisha na matangazo, uchapishaji na utengenezaji wa ‘video documentary’ mbalimbali, kwa filamu hiyo itakuwa ni ya kipekee hapa nchini na watu watafurahia.
Aidha, alisema kuwa filamu hiyo inatalajiwa kuzinduliwa katika uwanja wa Jamhuri Morogoro siku ya Idd Pili ambapo Cheka atakua na pambano kali dhidi ya bondia wa Uganda Sebyala Med.

No comments:

Post a Comment