b..

B1

Wynem

animation

Monday, August 23, 2010

MAMBO YA KCB HAYA!

Mwenyekiti wa Benki ya KCB Tanzania Dk Edmund Mndolwa akimkabidhi zawadi ya begi Mwanaidi Ibrahim ambaye alikuwa mmoja wa washindi wa michuano ya wazi ya gofu iliyodhaminiwa na benki hiyo katika hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya Gymkhana. Nyuma ni kepteni wa mchezo huo Joseph Tango. (Mpiga picha Wetu).
Mwenyekiti wa Benki ya KCB Tanzania Dk Edmund Mndolwa (Katikati) akimkabidhi Zainab Ibrahim zawadi fimbo ya mchezo wa gofu baada ya kuwa mshindi wa michuano ya wazi ya mchezo huo kwa upande wa wanawake iliyodhaminiwa na benki katika hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya Gymkhana. Anayeshuhudia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Gofu nchini (TGU) Dioniz Malinzi (Mpiga picha Wetu).
Mwenyekiti wa Benki ya KCB Tanzania Dk Edmund Mndolwa akihutubia wakati wa hafla ya kukabidhi zawadi za washindi wa mashindano ya wazi ya gofu yaliyodhaminiwa na benki hiyo.
Vikombe na baadhi zawadi za washindi wa mchezo wa gofu
Mchezaji wa Gofu ambaye pia ni mwanachama wa Dar es Salaam Club, Tayana William, akijiandaa kupiga mpira wakati wa mashindano ya wazi ya mchezo huo yaliyodhaminiwa na Benki ya KCB na kufanyika katika viwanja vya Gymkhana.
Christina Manyenye Mkuu wa Masoko na Uhusiano wa Jamii KCB kulia pamoja na wafanyakazi wenzie.


No comments:

Post a Comment