b..

B1

Wynem

animation

Thursday, August 19, 2010

NATURE AWAASA WASNII KUBADILIKA

Juma Kasim Nature

Baba Levo

"Nature" amewataka wanamuziki na wasanii wote nchini Tanzania kujali dhamana yao katika jamii,

Nature amesema "Wasanii na wanamuziki nchini wanayo nafasi kubwa ya kuibadili jamii na kuifanya iwe na maadili mema na kuendeleza utamaduni wake."

"Iwapo wasanii na wanamuziki hapa nchini watakumbuka wajibu wao na kuitekeleza kazi yao, jamii itanufaika,"alisema Nature.

"Ninawakumbusha wasanii na wanamuziki wenzangu hapa nchini kuachana na mazoea, Tuchape kazi kwa mujibu wa kazi yetu ya kuielimisha jamii yetu ya Kitanzania."

Mmoja wa wasanii wa kundi la TMK Wanaume Halisi maarufu kwa jina "Baba Levo" amesema wasanii na wanamuziki wengi wamejisahau kuwa hao ndio kioo cha jamii."
Kutokana na wasanii na wanamuziki kutembea sehemu mbalimbali wanaweza kuwa kiunganishi kizuri cha maendeleo kwa jamii iwapo hawatakuwa na roho za uchoyo.

No comments:

Post a Comment