b..

B1

Wynem

animation

Monday, May 23, 2011

WASHIRIKI WA MISS UNIVERSE WALIPOTEMBELEA OFISI ZA VODACOM

Meneja wa Bidhaa wa Vodacom Tanzania Joseline Kamuhanda akisalimiana na baadhi ya warembo wanaoshiriki shindano la Miss Universe walipotembelea makao makuu ya kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania ambaye ni moja ya mdhamni wa shindano hilo yaliyopo Mlimani City jijini Dar es Salaam
Mmoja wa warembo wa Miss Universe akipata maelekezo kutoka Omary Kilumanga ambaye ni Afisa wa Kitengo cha Mauzo kwa njia ya simu wa Vodacom Tanzania wakati washiriki wa shindano hilo lililodhaminiwa na Vodacom Tanzania walipotembelea makao makuu ya kampuni hiyo yaliyopo Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Mfanyakazi wa Vodacom Tanzania Kitengo cha Huduma kwa Wateja Laurent Ivo akiwaonesha baadhi ya warembo wanaoshiriki shindano la Miss Universe jinsi mfumo wa kitengo hicho unavyofanya kazi wakati washiriki wa shindano hilo lililodhaminiwa na Vodacom Tanzania walipotembelea makao makuu ya kampuni hiyo yaliyopo Mlimani City jijini Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment