b..

B1

Wynem

animation

Thursday, November 4, 2010

USALAMA WA TAIFA WAPINGA MADAI YA DK. SLAA.

Bw. Jacky Mugendi Zoka Naibu Mkurugenzi Idara ya Usalama wa Taifa akizungumza na waandishi wa habari leo katika mkutano uliofanyika kwenye hoteli ya Southern Sun jijini Dar es salaam wakati alipotoa taarifa ya kupinga madai ya Dk Willbrod Slaa Mgombea urais Kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kuwa idara hiyo imeshiriki katika kuchakachua Kura za mgombea huyo wa urais. Mkurugenzi huyo amesema wananchi wampuuze Dk Willbrod Slaa na kauli yake kwani madai yake hayana ukweli wowote na ameongeza kwamba idara yake haijajihusisha kabisa na masuala ya uchaguzi hivyo madai hayo ni ya kuipaka matope idara hiyo.

No comments:

Post a Comment