b..

B1

Wynem

animation

Monday, November 1, 2010

SHINDANO LA GIRAFE UNIQUE MODEL LAZINDULIWA RASMI LEO.

Mkurugenzi wa shindano la Urembo liitwalo Unique Modol, Bwa. Magessa akizungumza mchana huu katika moja ya kumbi za hoteli ya Giraffe jijini Dar,kuhusiana na uzinduzi wa shindano hilo linalotarajiwa kuanza hivi karibu.Miriam Gerald.
Hawa pia ni majaji kulia ni Mwakilishi wa Hoteli ya Girrafe Ocean View Gonza Muchunguzi na Mbunifu wa mavazi Ally Remtullah.
Baadhi ya wanahabari kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakiwa katika mkutano huo leo.


Kampuni ya Unique Entertainment imeandaa shindano la uanamitindo linalojulikana kama Unique Model litakalofanyika Desemba 24 mwaka huu katika hoteli ya Giraffe Ocean View. Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mkuu wa Unique Entertainment Methusale Magese alisema kuwa shindano hilo litajumuisha washiriki ishirini.
Alisema kuwa washiriki hao watapatikana katika mchujo utakaofanyika Novemba 20 mwaka huu katika hoteli ya Giraffe Ocean View. Aliwataja majaji watakaohusika katika mchujo huo kuwa ni mbunifu maarufu wa mavazi nchini Ally Rhemtulla, mwanamitindo Victoria Martin, Miss Tanzania 2009 Miriam Gerald na mcheza filamu maarufu Steven Kanumba.

Alivitaja vigezo vitakavyotumiaka katika shindano hilo kuwa ni urefu wa futi 5’ 8’-6’, hips 35-37, kiuno 26-29 na kifua 32-35.Vigezo vingine ni muonekano wa kiuanamitindo, kijiamini na umri 18-25, tabia njema na minato.Aliwataka wasichana wenye sifa hizo kujitokeza Giraffe Hoteli Novemba 20 kwa ajili ya mchujo kupata washiriki 20 watakaoingia kambini katika hoteli hiyo Desemba mwaka huu.

No comments:

Post a Comment