b..

B1

Wynem

animation

Tuesday, November 2, 2010

MAMBO YALIYOTOKEA KWENYE KIPINDI CHA MATOKEO KULE TANDIKA JIJINI DAR.

Hili ni gari la maji ya kuwasha likiwa tayari kwa lolote litakalotokea.
Raia wakiwa wamejichanganya na mawakala wa uchaguzi katika kituo cha polisi.
Palianza kuchafuka kihivi
Ikaja hivi
Polisi nao wakaanza kujisogeza.
Mapambano kati ya raia na polisi yalikuwa hivi.
Mwana habari akifuatilia habari kwa umakini.
Polisi wakafanikiwa kuwatia nguvuni baadhi ya raia kama wanavyoonekana katika picha
Mtaa mzima ukawa hauna utulivu mpaka Wafanyabiashara pia hapakukalika hivyo walilazimika kusitisha huduma kwa muda.Hivi ndivyo hali ilivyokuwa katika kitongoji cha Tandika mara baada ya kuchelewa kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi mkuu.Hali hiyo ambayo ililete mtafaruku mkubwa sana katika eneo hilo mpaka kupelekea jeshi la Polisi kufika katika eneo hilo na kuanza kutuliza ghasia zilizokuwa zikiendelea katika eneo hilo,ambapo maduka yalifungwa na wamiliki wake kulazimika kuondoka kabisa katika eneo hilo. Hadi mpiga picha wetu  anaondoka katika eneo hilo,ni kwamba mambo yalienda poa na vurugu ziliweza kudhibitiwa kabisa.

No comments:

Post a Comment