b..

B1

Wynem

animation

Thursday, October 28, 2010

ILIVYOKUWA KWENYE MKUTONO WA CHADEMA JANA JIJINI ARUSHA.

Umati Mkubwa wa watu uliofurika katika Viwanja vya NMC Arusha jana ukisikiliza Sera za Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA zilizokuwa zinatolewa na Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa (hayupo pichani) Bw, Freeman Mbowe ambaye pia ni Mgombea Ubunge Jimbo la Hai alipokuwa amelitembelea Jimbo la Arusha Mjini ili kuhamasisha kampeni za Chama chake wakati huu ambapo zimebakia siku chache kabla ya kupigwa kura za Uraisi, Ubunge na Udiwani Nchi nzima hapo Oktoba 31. katika Mkutano huo Mgombea wa nafasi ya Ubunge kwa Jimbo la Arusha Mjini Bw, Godbless Lema pamoja na Madiwani wote wa Chama hicho walipata nafasi ya kunadi Sera na kuomba kura
Wananchi wengi waliojitokeza kwenye Mkutano wa Pamoja wa Mgombea Ubunge Jimbo la Hai na Mgombea Ubunge Jimbo la Arusha Mjini wanaonekana wakiitikia Sera za Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema wakati wakisikiliza hutuba iliyokuwa inatolewa na Mwenyekiti wa Chama hichoTaifa Bw, Freeman Mbowe
Umati mkubwa wa watu ukiwasindikiza wagombea Ubunge kwa Majimbo ya Hai na Arusha Mjini kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA wakati walipokuwa wanaondoka katika Viwanja vya NMC Arusha jana baada ya kumaliza kuhutubia - Picha zote kwa Hisani ya Arusha Mambo.

No comments:

Post a Comment