b..

B1

Wynem

animation

Saturday, October 30, 2010

DR JAKAYA KIKWETE AHUBIRI AMANI NA KUWAONYA WATANZANIA WANAOENDEKEZA NA KUKUMBATIA UDINI!!

Jakaya Kikwete akiongea katika mkutano wake na waandishi usiku wa kuamkia leo ukumbi wa Anatouglou jijini Dar ambapo alihojiwa maswali mbalimbali juu ya mustakabali wa nchi endapo atachaguliwa kuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa awamu nyingine Uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani unafanyika Kesho Oktoba 31 nchini kote. Katika mahojiano hayo RaisDr. Jakaya Kikwete amewatahadhalisha watanzania kufanya maamuzi pasipo kuhubiri wala kuzingatia udini kwani kuzungumzia udini ni hatari na ni jambo litakaloigawa nchi kwa kiwango kikubwa na hakuna wa kutuokoa kwani hatuna pa kukimbilia kwakuwa nchi hii ni yetu hivyo tunatakiwa kuilinda na kuiheshimu ili tuishi kwa amani (Picha na Ankal Issa Michuzi)
Jakaya Kikwete na mgombea mwenza Dr Mohamed Gharib Bilali wakiondoka ukumbi wa Arnautoglou jijini Dar baada ya kuongea na waandishi wa habari usiku wa kuamkia leo.
Wahudhuriaji wakimsikiliza JK kwenye mkutano wake na waandishi wa habari katika ukumbi wa Arnautoglou jijini Dar usiku usiku wa kuamkia leo
Wahudhuriaji wakimsikiliza Jakaya Kikwete kwenye mkutano wake na waandishi wa habari katika ukumbi wa Arnautoglou jijini Dar usiku usiku wa kuamkia leo
Wahudhuriaji wakimsikiliza Jakaya Kikwete kwenye mkutano wake na waandishi wa habari katika ukumbi wa Arnautoglou jijini Dar
Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu Bw. Salva Rweyemamu akimuamkia Dk. Mohamed Ghalib Bilali kabla ya kuanza kwa mkutano wa Jakaya Kikwete na waandishi usiku wa kuamkia leo ukumbi wa Arnautoglou jijini Dar
Jakaya Kikwete akiwashukuru watangazaji wa TV mbalimbali waliokuwa wakimhoji kwenye mkutano na waandishi usiku huo kwenye ukumbi wa Arnautoglou jijini Dar
Jakaya Kikwete akisalimiana na waandishi na wageni waalikwa kwenye mkutano wake na waandishi ukumbi wa Arnautoglou jijini Dar
Hassan Mhelela wa BBC London akimhoji mgombea mwenza wa urais Tanzania bara Dk. Mohamed Gharib Bilal baada ya mkutano wa JK na waandishi usiku wa kuamkia leo ukumbi wa Arnautoglou jijini Dar
Hassan Mhelela wa BBC London akimhoji Makamu Mwenyekiti wa CCM Mh. Pius Msekwa baada ya mkutano wa JK na waandishi wa habari
Fundi mitambo mkuu wa Clouds TV Mehboub al Hadad akiwa kazini ambapo kituo hicho kiliungana na vingine kurusha mkutano wa JK na waandishi live
Baadhi ya wahariri wa vyombo mbalimbali wakimsikiliza JK akijibu maswali usiku wa kuamkia loe katika ukumbi wa Arnautoglou jijini Dar

No comments:

Post a Comment