b..

B1

Wynem

animation

Monday, December 19, 2011

RAIS JAKAYA KIKWETE AWAAPISHA MABALOZI WAPYA IKULU DAR ES SALAAM LEO


 Rais Jakaya Kikwete, akimwapisha, Phillip  Marmo, kuwa Balozi wa China, wakati wa hafla fupi ya kuwaapisha mabalozi wapya iliyofanyika mchana huu, Ikulu Dar es Salaam. Marmo awali alikuwa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge.
 Mabalozi wapya waliofia Ikulu Dar es Salaam leo kwa ajili ya kuapishwa na Rais Jakaya Kikwete, wakisubiri kuapishwa.
 Rais Jakaya Kikwete, akimwapisha, Dkt. Batilda Buriani,  kuwa Balozi wa Kenya, wakati wa hafla fupi ya kuwaapisha mabalozi wapya iliyofanyika mchana huu, Ikulu Dar es Salaam. Batilda awali alikuwa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira). 
 Rais Jakaya Kikwete, akimwapisha, Dkt. Deodorus Kamala, kuwa Balozi wa Ubelgiji, wakati wa hafla fupi ya kuwaapisha mabalozi wapya iliyofanyika mchana huu, Ikulu Dar es Salaam. Kamala, awali alikuwa ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
 Rais Jakaya Kikwete, akimwapisha, Ally A. Saleh, kuwa Balozi wa Oman, wakati wa hafla fupi ya kuwaapisha mabalozi wapya iliyofanyika mchana huu, Ikulu Dar es Salaam. Saleh, awali alikuwa ni Balozi Mdogo wa Dubai.
 Rais Jakaya Kikwete, akimwapisha, Shamim Nyanduga, kuwa Balozi wa Msumbiji, wakati wa hafla fupi ya kuwaapisha mabalozi wapya iliyofanyika leo mchana huu, Ikulu Dar es Salaam. Nyanduga awali alikuwa ni Naibu Mkuu wa Itifaki, Wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
 Samim Nyanduga, akipongezwa na Mumewe, baada ya kuapishwa rasmi kuwa Balozi wa Msumbiji, wakati wa hafla hiyo iliyofanyika Ikulu Dar es Salaam leo. Nyuma yao ni wanafamilia wa Familia hiyo.
 Rais Jakaya Kikwete, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal (kushoto), Waziri  Mkuu, Mizengo Pinda (kuli) na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe, wakizungumza jambo, baada ya kumalizika kwa hafla fupi ya kuwaapisha mabalozi wapya iliyofanyika Ikulu Dar es Salaam leo.
Rais Jakaya Kikwete, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Waziri  Mkuu, Mizengo Pinda, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani na Ushirikiano wa Kimataifa, Mahadhi Juma Maalim, wakiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wapya baada ya kuapishwa rasmi leo Ikulu Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment