b..

B1

Wynem

animation

Friday, May 25, 2012

CAMP MULLAH WAPATA HARUFU YA MABILIONI YA CHRIS KIRUBI

Kundi la CAMPMULLAH la nchini Kenya
Chris Kirubi - Mmoja kati ya mabilionea wa Afrika
Nyota ya kundi la Hip hop la Campmulla la Kenya inazidi kung’aa. Juzi tu walipokea habari njema ambayo tayari imewaweka kwenye historia ya muziki wa Afrika Mashariki kwa kutajwa kwenye tuzo za BET kwenye kipengele cha Best International Act Africa. Na sasa tajiri namba 31 katika orodha ya matajiri barani Afrika kwa mujibu wa Forbes Magazine anataka kuwapa shavu?? Si mwingine ni tycoon wa nchini Kenya Chris Kirubi ambaye ni mmiliki wa Capital FM ya Kenya. 
Ilikuwa ni baada ya leo kufanya interview Capital FM na Lora Walubengo,kama bahati vijana hao watano wakakutana na Mr. Kirubi kubadilishana story mbili tatu! Baada ya kuachana, Kirubi ambaye ni mhudhuriaji mzuri wa mitandao ya kijamii, akatweet, “@CampMulla Great meeting you guys, I think the future is very bright for you. We will work together. Just stay on course."
Ukiambiwa “we will work together. Just stay on cource” na mtu ambaye utajiri wake unafikia $300 Million! Lazima ushtuke kidogo, ushushe pumzi, utulie na kisha ucheke kimoyomoyo na kuimba ‘money, money, money’! 
Kwa umaarufu walionao CampMulla kazi zipo nyingi tu za kufanya na Chris Kirubi husasan zinazohusu kupromote biashara zake. Anamiliki jengo ambalo ni miongoni mwa majengo marefu na yenye thamani zaidi jijini Nairobi! Ni mmiliki wa shirika kubwa la bima, UAP Insurance na kampuni ya ujenzi ya Sandvik East Africa pamoja na michongo mingine!

No comments:

Post a Comment