b..

B1

Wynem

animation

Friday, February 18, 2011

WAATHIRIKA WA MABOMU YA GONGO LA MBOTO WAENDELEA KULETWA UWANJA WA UHURU.



Mama wa watoto wa tatu aliejitambulisha kwa jina la Zawadi Hassan akiwa na watoto wake wawili huku akihuzunika kwa kutokujua alipo mtoto wake mmoja wapo kutokana na kukimbia kwa kujinusuru na mabomu yaliyokuwa yakilipuka usiku wa kuamkia leo huko gongo la mboto.
Sehemu ya watoto waliookotwa huko Gongo la Mboto wakiwa ndani ya gati wakati wakiletwa ndani ya uwanja wa Uhuru jijini Dar mchana huu.
wengine wakiendelea kuletwa hivi sasa.
Uandikishaji ukiendelea kwa wahanga wa mabomu ya huko Gongo la Mboto.
Wengine wakiwa wamejipumzisha kutokana na uchovu wa usiku kucha kwa hali iliyokuwa huko Gongo la Mboto kutokana na Milipuko ya mabomu katika moja ya maghala ya kambi ya Jeshi la Wananchi (JWTZ) iliopo huko Gongo la Mboto usiku wa kuamkia leo.
Wadau wa Msalaba Mwekundu wakiendelea kutengeneza mahema ya kuhifandhia wahanga wa mabomu yaliyoripuka usiku wa kuamkia leo na kusababisha watu wengi kupoteza makazi yao.
Mmoja wa wasamalia aliejutokeza uwanjani hapo akiwa pamoja na kijana wa Scout wakiwasaidia kuwanywesha maziwa watoto waliletwa uwanjani hapa kutokana na kupoteana na wazazi wao.
hali bado si shwari huko Gongo la Mboto kwani bado idadi kubwa ya watoto na wakazi wa maeneo hayo wanaendelea kuletwa uwanjani hapa.

No comments:

Post a Comment