b..

B1

Wynem

animation

Monday, February 7, 2011

LISTENING SESION YA THE ELEMENT MIXPATE KUWAUNGANISHA WADAU

Tarehe 23 mwezi huu, itafanyika bonge la listening session ya THE ELEMENT MIXPATE pale mzalendo pub. Na baadhi ya wageni watakaofanya siku hiyo ikamilike ni pamoja na DJ PQ, Fid Q na wengine kibao ambao watatajwa kadiri siku inavyokwenda (ikikaribia). Nia ya Listening session hii si tu kwa ajili ya kusikiliza mixtape hii bali pia kama sehemu ya kuunganisha wadau na kubadilishana mawazo katika mambo tofauti tofauti. Pia kutakuwa na SHOWCASE ya djs wachanga kwa wale watakaotaka kuji expose katika industry, pia utaratibu wa namna hiyo hiyo kwa Young Producers kufanya showcasing inayoweza kuwaunganisha na wasanii wakubwa katika siku hiyo. kwa kufanikisha hili na pia kuchochea mwamko wa siku hiyo. basi tumeamua ku release track namba moja katika MIKS TAPE hii ukienda wka jina la HISIA.
Ni track pekee ambayo wahusika wakuu katika huu mzigo wameunganika pamoja, ni track inayozungumzia changamoto mbali mbali katika maisha yetu ndani ya jamii.... Verse I: Nikki anaelezea changamoto zinazokabiliwa kwenye game la music wetu.... Verse II: STEREO kajikita na changamoto za mtaani na mambo ya uswahilini, VERSE III: SUMA yeye kajitosa katika changamoto za utapeli wa mapenzi Verse IV: ONE THE INCREDIBLE yeye kaingia ndani ya familia zilizokosa mwelekeo.
Ni track ambayo haina chorus, 32 bars each, tunahisi inaweza isiwe ni user friend sana kwa media kwa sababu za itikadi za kibiashara (ni NYEUSI its not commercial) lakini ina ujumbe mkubwa ndani yake....bado tunaamini na ku project kuwa itakuwa na impact kubwa sana mtaani zaidi na kwenye net kuliko kwenye radio .
Hii track ni ruksa kuipiga kwa radio, kuisambaza thru NET na hata mtaani...lengo ni kufikisha ujumbe katika hadhira ya kitaani zaidi.
SIKILIZA WIMBO HUU KWENYE PLAY LIST HAPO KULIA KWAKO

Track: Hisia
Artist: Nikki Mbishi, Stereo, Suma & One
Produced by Duke
The Element mixtape
Music Lab 2011.

Patrick,
Artists & Studio manager,

Media Kings Tanzania Limited-Music Lab

No comments:

Post a Comment