Hapa mwana wa kitaa nilifika katika ofisi za serikali ya mtaa wa tandale kwa tumbo na nilipokelewa vizuri na uongozi ambao walitupa mwenyeji wa kutuzungusha kila kona na kuweza kuongea na wananchi tofautitofauti.
Hawa ndio vingozi wenyewe wa mtaa.
Tukapita pita mitaani bana na hapa ni makazi ya watu. Huyu mshkaji anaitwa Nassoro Mzee ndio alikuwa mwenyeji wetu.
kama kawaida mtotowa kitaa ni mpenzi wa watoto na pia napendwa na watoo hivyo watoto hawakua nyuma katika kunipa kampani
pia nilipita mahali ambapo unaweza kuona mazingira ya upande mwingine huku pakiwa pametenganishwa na bonde kubwa ambalo pia ni mkondo wa maji.
nikaendelea kukata mitaa.
hiki ndio choo kinachotumika na moja kati ya kaya (nymuba) pande za tandale
Mazingira ndio kama yanavyoonekana
Mimi niakchoka bana ikabidi mwanangu tulio ongozana nae aendelee na mchakato mzima. Alex Peter Nyaganilwa (father P) akiongea na bibi anaeishi tandale.
Tulifika mahali ikabidi tupumzike kwa maana uchovu wa mzunguko ukiuchanganya na mfungo yaani ni balaaa!
No comments:
Post a Comment