b..

B1

Wynem

animation

Friday, September 17, 2010

WATUMIAJI WA VODACOM SASA WAPATA AHUENI.

Vodacom Tanzania imepunguza gharama zake katika huduma ya kupiga simu, ambapo wateja wa Vodacom wataweza kupiga simu kwenda mitandao mingine nchini kwa punguzo la zaidi ya asilimia 50.Hii ni katika jitihada za kampuni hii kuhakikisha kuwa mawasiliano yanapatikana kwa gharama nafuu, nchi nzima.
Gharama hizi mpya zitamruhusu mteja wa Vodacom kuweza kupiga kwenda mitandao mingine kwa kiasi kidogo cha shilingi tatu tu za kitanzania kwa sekunde, wakati hapo awali gharama ya kupiga simu kwenda mitandao mingine ilikuwa shilingi sita na nusu.
Huduma hii imekuja miezi michache tu baada ya Vodacom kuzindua huduma nyingine ya shilingi moja kwa sekunde , maarufu kama HABARI NDIO HII.
Ikiwa na wateja milioni nane nchini, kampuni ya Vodacom imeendelea kutoa bidhaa na huduma kwa wateja wake,na kuwawezesha kupata mawasiliano kwa gharama nafuu.
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Vodacon Tanzania, Mwamvita Makamba alisema jana kwamba kuwa gharama hizi mpya zimeleta mapinduzi katika sekta ya mawasiliano ya simu nchini.
“Kama tulivyozindua huduma ya Habari Ndio Hii, tumejikita kuhakikisha kuwa mtandao wetu unatoa bidhaa na huduma bora kwa wateja wetu ili kuwajenga kiuchumi.”
Kampuni ya Vodacom imekuwa nchini kwa miaka kumi sasa na inatabiri kukua zaidi katika sekta hii mwaka huu na miaka mingine ijayo.
“Tutamatumaini makubwa juu ya utendaji wetu hapo mbeleni na tunashauku kubwa kuweza kutoa huduma zetu zenye ubora wa hali ya juu kwa gharama nafuu.”
Huduma zingine za Vodacom kama Vodajamaa na Cheka Time zitabaki kama zilivyo.
“Vodacom inawahakikishia wateja wake kuwa itaendelea kutoa huduma zenye ubora wa hali ya juu hapo mbeleni” Bi Pendaeli alihitimisha kusema.

No comments:

Post a Comment