b..

B1

Wynem

animation

Tuesday, June 23, 2015

BONDIA WA KIKE, MWANNE HAJI AWATAKA MABONDIA DAR

Na Mwandishi Wetu 
BONDIA wa kike Mwanne Haji ambaye amejitokeza kupambana na mabondia kwa kike wa Dar es salaam baada ya kuwasumbua sana mabondia wenzake wanaotoka Chunya Mkoa wa Mbeya na sasa kujikita jijini akitokea katika GYM ya Zugo iliyopo Gongolamboto.
Bondia huyo wa kike ambaye ameshapanda ulingoni kupambana na baadhi ya mabondia wa mkoani, amesema amekuja kwa ajili ya mchezo wa masumbwi jijini. Hivyo mabondia wa kike wakae pembeni kwani sasa ata wasambaratisha mmoja baada ya mwingine alitolea mfano wa mabondia wanaotamba Dar es salaam kwa kupigana wenyewe kwa wenyewe kila wakati ni Lulu Kayage, Halima Ramadhani, Fatuma Yazidu.
Sasa wakae foleni kwani atawapa vipigo mmoja baada ya mwingine bondia uyo mpaka sasa amecheza michezo mitatu ambapo mchezo wake wa kwanza alicheza na Vailet Modest na kufanikiwa kumtwanga kwa point mchezo wake wa pili alicheza na Telesia Kiwale na mchezo wake wa tatu alicheza na Jennifer Pius na kumsambalatisha kwa pointi.
Hivyo amewaomba mapromota wajitokeza kumsaidi kupambanishwa na mambondia aliowataja hapo juu kwa uzito wa kg 49.
Mbali na hivyo ametowa wito kwa tasisi mbalimbali pamoja na kmpuni kujitokeza kudhamini mchezo wa masumbwi kwani unapendwa na mashabiki lukuki nchini.


Super D Boxing Coach
 Mob;+255787 406938
        +255713 406938 
        Po.Box. 15493
Dar es Salaam Tanzania

No comments:

Post a Comment