b..

B1

Wynem

animation

Sunday, June 28, 2015

JANUARY MAKAMBA AMALIZA KAZI ARUSHA MJINI, WANANCHI WAMFAGILIA KWA HOTUBA NA MIPANGO YAKE, WAMTAKIA USHINDI MNENE

Mbunge wa Bumbuli na naibu waziri wa mawasilano, sayansi na teknolojia, January Makamba akisalimiana na wananchi na wananchama wa CCM mkoa wa Arusha waliojitokeza katika viwanja vya ofisi za CCM mkoa kumuunga mkono katika harakati zake za kusaka wadhamini mkoani hapo. January amejizolea wadhamini 2227 kutoka mkoa huo.

Mbunge wa Bumbuli na naibu waziri wa mawasilano, sayansi na teknolojia, January Makamba akiweka sahihi kwenye kitabu cha wageni katika ofisi ya katibu wa CCM mkoa wa arusha mara baada ya kuwasili mkoani hapo kwa ajili ya kuomba udhamini wa wanachama wa CCM utakaomuwezesha  kuteuliwa kuwania nafasi ya urais wa Tanzania kupitia tiketi ya CCM. Ambapo mkoani Manyara amepata wadhamini 2227. Kushoto ni mke wake, Ramona Makamba.

Mbunge wa Bumbuli na naibu waziri wa mawasilano, sayansi na teknolojia, January Makamba akiwapungia mkono wananchi na wananchama wa CCM mkoa wa Arusha alipokuwa akiingia ukumbini kuhutubia na kuomba udhamini wa wanachama hao ili kupata ridhaa ya chama kuteuliwa na chama kugombea nafasi ya urais. Mbele kabisa na katibu wa CCM arusha Mjini, Feruzy Bano

Katibu wa CCM arusha Mjini, Feruzy Bano akimkabidhi mh January Makamba fomu yenye majina na sahihi za wanachama wa CCM waliomdhamini katika Ukumbi wa CCM mkoa wa Arusha. January amepata wadhamini 2227.
Mbunge wa Bumbuli na naibu waziri wa mawasilano, sayansi na teknolojia, January Makamba akionyesha  fomu yenye majina na sahihi za wanachama wa CCM waliomdhamini katika Ukumbi wa CCM mkoa wa Arusha. January amepata wadhamini 2227.

Mh January Makamba akihutubia wananchi na wanachama wa CCM mkoani Arusha waliojitokeza katika Ukumbi wa ndani wa CCM mkoa wa Arusha. January yupo katika ziara yake ya kusaka wadhamini ndani ya chama ambao watamuwezesha kuteuliwa kuwania nafasi ya urais wa Tanzania kupitia tiketi ya CCM. Ambapo mkoani Manyara amepata wadhamini 2227.
Baadhi ya wananchi na wanachama wa CCM mkoa wa Arusha wakiwa wanafuatilia hutuba ya mh January Makamba  nje ya ukumbi wa CCM mkoa kupitia Runinga maalumu zilizokuwa nje ya ukumbi huo, Januray alihutubia wananchi na wanachama wa CCM mkoa wa Arusha ambapo alipata wadhamini 2237 kwa mkoa huo.

Mbunge wa Bumbuli na naibu waziri wa mawasilano, sayansi na teknolojia, January Makamba akijibu baadhi ya maswali yaliyoulizwa na wananchi wa jiji la Arusha kwenye mkutano uliofanyika katika ukumbi wa CCM mkoa wa Arusha jana. Picha zote na Mpigapicha wetu.

No comments:

Post a Comment