b..

B1

Wynem

animation

Monday, April 29, 2013

EXTRA BONGO YAZIDI KUWABAMBA MASHABIKI NDANI YA MEEDA SINZA JANA USIKU

Mkurugenzi wa Extra bongo Ally Choki akiimba mbele ya mashabiki wake (Hawapo Pichani) ndani ya Ukumbi wa Meeda sinza jana Usiku wakati bendi yake ilipokuwa ikiburudisha pande pande hizo
Kushoto ni mmoja wa marapa bora wa muziki wa dansi Totoo Ze Bingwa akirap ndani ya Meeda sinza wakati Bendi anayopigia mzigo Extra Bongo ilipokuwa ikitumbuiza pande hizo na kulia ni Banza Stone a.k.a Generale akimpa big up.
Rapa bora wa Extra bongo Kabatano (Kulia) akigani moja ya jimbo zao bora huku akipewa sapoti na nguli wa muziki wa dansi Banza Stone mwana masanja wakati bendi hiyo ilipokuwa ikitumbuiza maeneo ya Sinza katika ukumbi wa Meeda jana usiku.
Wakata nyonga maarufu kwa sasa wa Extra bongo wakiongozwa na nyamwela wakiwapagawisha mashabiki waliohudhuria shoo hiyo ndani ya Meeda Sinza jana usiku

No comments:

Post a Comment