b..

B1

Wynem

animation

Thursday, August 16, 2012

AIRTEL YATANGAZA SHULE 93 ZA SEKONDARI ZITAKAZO FAIDIKA NA MRADI WA VITABU.

Mkurugenzi mkuu wa mawasiliano Beatrice Singano (katikati), Meneja huduma kwa jamii wa Airtel Bi, Hawa Bayumi (kulia) na Bw Masozi Nyirenda, wakionyesha vitabu vilivyotolewa na Airtel
Mkurugenzi mkuu wa mawasiliano Beatrice Singano akiongea na waandishi
wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla maalum ya Mradi na droo ya
kugawa Vitabu kwa Shule za Sekondari ijulikanoyo kama ‘ AIRTEL SHULE YETU’ iliyofanyika katika ofisi za Airtel. Kulia ni Meneja huduma kwa jamii wa Airtel Bi, Hawa Bayumi na kushoto ni Ofisa Mkuu Mwandamizi wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) Bw Masozi Nyirenda.

Na Mwandishi wetu
Dar as Salaam, Airtel Tanzania, imeendeleza dhamira yake katika kuboresha elimu kwa kuchezesha droo iliyochagua shule za sekondari  93
zitakazo faidika na mradi wa vitabu wa Airtel wa kusaidia jamii unaojulikana kama  Airte shule yetu kwa  mwaka 2012 -2013. Akiongea katika mkutano na vyombo vya Habari Mkurugenzi wa Airtel Kitengo cha Mawasiliano Bi, Beatrice Singano Mallya alisema “Mwaka huu, Airtel tunaendelea na dhamira yetu ya kusaidia elimu kwa kuzipatia vitabu shule  za sekondari 93.
Mradi huu utafaidisha shule 3 kutoka katika kila mkoa Tanzania bara na visiwani.
Shule 93 zilizochaguliwa ni matokeo ya droo iliyochezeshwa na kuzichagua shule hizo kutoka shule 3,000 zilizopendekezwa na Wizara ya Elimu Tanzania kuwa ni shule ambazo zina uhitaji mkubwa wa vitabu na kushauri  ziingie katika mpango wa kusaidia jamii wa Airtel shule yetu.
“Toka tulivyooanza mradi huu wa Vitabu miaka saba iliyopita tumeweza kuzifikia zaidi ya shule 1000 za sekondari zilizopo Tanzania bara na visiwani  kwa kutoa msaada sawa kwa mikoa  yote  na kuwafikia wanafunzi katika kila kona ya Tanzania.
Mwaka huu vitabu tunavyogawa vinakadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya shilingi milioni 110, hivyo kila shule  iliyopatikana kwenye droo hii watapata Vitabu alisema Mallya.
Bi Mallya aliongeza kwa kusema “tumefanya kazi kwa pamoja na Mamlaka ya elimu na Wizara ya Elimu Tanzania kwa kuhakikisha kwamba mahitaji ya vitabu kwa shule zote zitakazoingia kwenye Mradi huu wa Shule yetu tunayatimiza kwa  kuwapatia vitabu vya mitaala ya  masomo yao kama ilivyopendekezwa na Wizara” 
“Airtel Tanzania imekuwa mstari wa mbele kwa kutoa misaada mbalimbali ili kuisaidia jamii hapa Tanzania  hasa kwa kuchangia sekta ya elimu kwa kuwapatia vitendea kazi vikiwemo Vitabu  kwa wanafunzi wa shule za sekondari.
Mwaka jana pia Airtel ilisaidia Vitabu vyenye thamani ya zaidi ya milioni 104 tsh  kwa  shule za sekondari kwa kupitia  droo iliyohusisha jumla ya shule 502″ alisema Bi, Mallya.

Nae Afisa Mkuu Mwandamizi wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) Bw Masozi Nyirenda aliongea kwa Niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Ulimu (TEA) alisema “Mamlaka ya Elimu Tanzania tunawashukuru sana Airtel kwa dhamira yenu ya kusaidia jamii kwa kuinua kiwango cha elimu hapa nchini” Mradi wa Airtel Shule Yetu ni mradi mzuri sana kwa jamii yetu kwa kuinua kiwango cha elimu  na maisha ya watanzania”.
Tunaamini elimu ndio ufunguo wa maisha hivyo watanzania wote pamoja na waalimu mtakaopokea vitabu hivi vya mradi wa Airtel Shule yetu tuvitunze na kuvitumia vizuri ili kuunga mkono jitihada za Airtel katika kusaidia kuinua kiwango cha elimu hapa nchini” aliongeza kwa kusema Bw, Nyirenda.
Mbali na  shule 93 za sekondari zitakazofaidika na mradi huu wa vitabu mwaka huu,  pia Airtel Tanzania imeshamaliza kukarabati shule ya msingi ya Kiromo iliyopo nje kidogo ya jiji la DSM kando kando na barabara ya bagamoyo  ilichaguliwa mwaka jana 2011 huku mipango mingine ya mwaka huu ikiendelea ili kupata shule nyingine itakayofaidika kwa kujengwa na kukarabatiwa na Airtel shule Yetu.
Airtel bado itaendelea kushirikiana wizara ya elimu kwa wadau wengine kuweza kushiriki katika kuinua kiwango cha elimu hapa Tanzania.

No comments:

Post a Comment