b..

B1

Wynem

animation

Thursday, January 16, 2014

NGUMI KUPIGWA MKOA WA PWANI IJUMA


Na Mwandishi Wetu
NGUMI kupigwa mkoa wa Pwani  mchezo wa masumbwi unatarajia kufanyika siku ya ijumaa katika ukumbi wa Shimbikati  pub uliopo Kiluvya Mkoa wa pwani mpambano  mchezo wa ngumi katika mkoa wa pwani umendaliwa na kocha wa mchezo huo Jafar Ndame
akizungumzia mpambano huo ambao unasubiliwa kwa hamu na wakazi wa kiluvya pamoja na vitongoji vyake litawakutanisha mabondia Azizi Abdallah atakaepambana na Sadam Manjapa uku Julius Kisarawe akivaana na Haji Gamba, na Tasha Mjuaji akimkabiri roja mjeshi na mapambano mengine mengi ya utanguliza pamoja na burudani nyingine nyingi
Mipambano hiyo ya masumbwi yatakuwa chini ya chama cha ngumi za kulipwa PST na Rais wake Emanuel Mlundwa ambao ndio wasimamizi wakuu wa mchezo huo siku hiyo
mbali na kuwepo kwa mchezo huo wa masubwi pia kutakuwa na huzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi wakiwemo mabondia wak
ali kama vile Floyd Maywether,Manny Paquaio,Oscar Dela Hoya,Mohamed Ali,mike Tyson, pamoja na mabondia mbalimbali pia kutakuwa na vifaa vya mchezo wa masumbwi kama vile glove,gumshiti,clip bandeji na vifaa mbalimbali vitakavyokuwa vikiuzwa na kocha wa kimataifa wa mchezo wa masum,bwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' kwa ajili ya kuhamasisha mchezo huo ili wapenzi wajue sheria na taratibu za mchezo wa masumbwi

No comments:

Post a Comment