b..

B1

Wynem

animation

Monday, December 3, 2012

BAGAMOYO, MKOA WA PWANI WAHAMASISHA NGUMI KWA KISHINDOMKOA


Bondia Zumbe Kikuru kushoto akipambana na Toma Kato wakati wa mpambano wao uliofanyika katika ukumbi wa Saadan High Way Bagamoyo mwishoni mwa wiki iliyopita Kikuru alishinda kwa  K'O raundi ya pili 

Mashabiki waliojitokeza kushudia mpambano wa masumbwi uliofanyika katika ukumbi wa Saadan High Way Bagamoyo mwishoni mwa wiki iliyopita.
Refarii wa mpambano wa masumbwi Said Chaku katikati akimwinua mkono juu bondia Obete Ameme baada ya kumtwanga mpinzani wake katika raundi ya kwanza kwa K,O uliofanyika katika ukumbi wa Saadan High Way Bagamoyo mwishoni mwa wiki iliyopita.
Picha Zote na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Na Mwandishi Wetu
Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa Masumbwi nchini anaefundisha Timu ya Ashanti pamoja na timu ya Mkoa wa Ilala Kimichezo Rajabu Mhamila 'Super D' amevutiwa na mashabiki wa mchezo huo mkoa wa Bagamoyo Pwani
Baada ya kuvutiwa na umati mkubwa uliojitokeza katika mpambano uliofanyika Bagamoyo mkoa wa pwani mwishoni mwa wiki iliyopita mpambano uliofanyika katika ukumbi wa Saadan High Way ambapo uliudhuliwa na mashabiki wengi wa bagamoyo
Kocha huyo anaefundisha kwa njia mbalimbali ikiwemo DVD amevutika kwa wapenzi wa ngumi bagamoyo kuchangamkia DVD hizo zenye kuelimisha mchezo wa masumbwi pamoja na kujua shelia mbalimbali za ngumi Duniani
Mpambano huo ulioandaliwa na Sharif Muhsin na kuratibiwa na bondia wa siku nyingi Said Yazidu umefungua ukurasa mpya kwa wakazi wa bagamoyo kuukubali mchezo huo na kuendelea kuupenda na kuwapa sapotimabondia wanaowakilisha Bagamoyo
Baazi ya mabondia waliopigana katika mpambano huo ni Maneno Zele alipata kichapo kutoka kwa Baisa Juma wakati Zumbe Kikuru alimtwanga kwa K,O Tomo Kato katika raundi ya kwanza huku Kadani Rhamwana alimchapa Ndumbo Hassani kwa point 
Mpambano huo ni wa pili kufanyika kwa mwaka huu umendelea kuwa chachu ya kupata vipaji vipya vya mchezo wa ngumi hapa nchini

No comments:

Post a Comment