b..

B1

Wynem

animation

Friday, July 31, 2015

NGUMI KUPIGWA TENA VIJANA KINONDONI SEPTEMBA 6


B0NDIA Mbena Rajabu atapanda tena uringoni kuzidunda na Twaribu Mchanjo mpambano utakaofanyika Septemba 6 katika ukumbi waVijana Kinondoni kugombania ubingwa wa Taifa wa uzito wa kg 57

mpambano uho unaoratibiwa na Ibrahimu Kamwe utakuwa na mapambano mengine ya utangulizi yatakayowakutanisha mabondia mbalimbali nchini ambapo bondia Abdallah Pazi atazidunda na Ambokile Chusa na Georger Alen wa Muheza Tanga atazipiga na Mwinyi Mmzengela  wakati Epson John wa Morogoro atazidunda na Mohamed Alkaida 

Kamwe aliongeza kwa kusema mpambano uho ameuandaa kwa kuakikisha wanakuwa na mabondia wengi ambao watakuwa mabingwa na kuwakilisha nchi katika mapambano mbalimbali ya kitaifa na kimataifa

Katika mpambano huo siku hiyo kutakuwa na uzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi  kali pamoja na kutambua sheria zake zikiwa na mabondia wakali kama vile
Floyd Mayweathar, Manny Paquaio, Saul 'canelo' alverez, Mike Tyson, Mohamed Ali, Ferex Trinidad, Miguel Cotto na wengine wengi
pia kuta kuwa na vifaa vya mchezo vitakaokuwa vikitolewa na Rajabu Mhamila 'Super D' kwa mabondia watakaofanya vizuri siku hiyo na vingine kuuzwa kwa pesa taslimu na kocha huyo kwa ajili ya kuamasisha

No comments:

Post a Comment