b..

B1

Wynem

animation

Friday, June 3, 2016

NGUMI ZA KIMATAIFA KUPIGWA KESHO UWANJA WA NDANI WA TAIFA JUNI 4

Mabondia Vicent Mbilinyi kushoto akitunishiana misuli na Msafili Haule baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambao wao utakaofanyika katika uwanja wa ndani wa Taifa siku ya jumamosi ya juni 4.
Promota wa mkanda wa ubingwa wa Dunia wa U.B.O Juma Ndamile kushoto akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kutangaza mpambano uho pamoja na upimaji uzito kwa mabondia wengine ni Kulwa Makaranga na bondia Cosmas Cheka atakaegombania ubingwa wa Dunia na Chrispin Moliyati mpambao wao utakaofanyika katika uwanja wa ndani wa Taifa siku ya jumamosi ya juni 4.
Bondia Lulu Kayage kushoto akitunishiana misuli na mpinzani wake Will Enelesi wa Malawi mpambano wao utafanyika juni 4 katika uwanja wa ndani wa Taifa 
Bondia Ashiraf Selemani kutoka Zanzibar  kushoto akitunishiana misuli na ElickGogodo wa Malawi baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao utakaofanyika kesho katika uwanja wa ndani wa Taifa.
Bondia Alphonce Mchumiatumbo kushoto akitunishiana misuli na Mussa Ajiba baada ya kupima uzito kwa ajili ya Mpambano wao utakaofanyika kesho katika uwanja wa ndani wa Taifa
Mabondia Vicent Mbilinyi kushoto akitunishiana misuli na Msafili Haule baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambao wao utakaofanyika katika uwanja wa ndani wa Taifa siku ya jumamosi ya juni 4
Mabondia Vicent Mbilinyi kushoto akitunishiana misuli na Msafili Haule baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambao wao utakaofanyika katika uwanja wa ndani wa Taifa siku ya jumamosi ya juni 4 

Picha zote na SUPER D BOXING NEWS



Na Mwandishi Wetu
BONDIA Cosmas chka anapanda uringoni kugombania ubingwa wa Dunia wa U.B.O kwa kupambana na Chrispin Moliyati kutoka Malawi mpambano wa raundi 12 wakisindikiza na mabondia chipkizi ambapo bondia kutoka katika kambi ya 'Super D' Vicent Mbilinyi ata kabiliana na bondia kutoka kambi ya akina ukoo wa Matumla Msafili Haule watazipiga katika uzito wa kg 63 mpambano wa raundi 6.
Mipambano mingine ya kimataifa yaa wakutanisha mabondia wa kike Lulu Kayage wa Tanzania atakaezipiga na Will Eneles kutoka Malawi
wengine ni Japhert Kaseba atazidunda na Amour Mzungu kutoka Zanzibar na Ashiraf Selemani kutoka Zanziba atakumbana na Elick Gogodo wa Malawi katika mchezo wa uzito wa juu kabisa wakati Alphonce Mchumiatumbo atakabiliana na Mussa Ajibu kutoka Malawi mpambano wa raundi sita

siku hiyo kutakuwa na burudani mbalimbali zitakazo sindikiza mapambano hayo ya kimataifa ya mchezo wa masumbwi pia ngumi zitaanza mapema kuepusha usumbufu unaojitokezaga kwa wapenzi kuchelewa majumbani mwao kwa ajili ya mchezo wa masumbwi

siku hiyo pia kutakuwa na ugawaji wa zawadi kwa mabondia watakaocheza vizuri na kuonesa nidhamu ya mchezo wa masumbwi ikiwemo vifaa vya mchezo pamoja na DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi pamoja na kutamba sheria za mchezo uho nyingine zitakuwa zikiuzwa kwa galama nafuu kwa mashabiki watakaofika siku hiyo.

No comments:

Post a Comment