b..

B1

Wynem

animation

Monday, December 22, 2014

BONDIA TWAHA KASSIM WA MOROGORO AMTWANGA KWA KO, MUSSA CHITEPETE WA SONGEA

Mabondia Twaha Kassim wa morogoro kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Mussa Chitepete wa Songea wakati wa mpambano wao uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Kassim alishinda kwa K,O ya raundi ya sita 
Bondia Mussa Chitepete wa Songea akiwa chini baada ya kupokea konde zito kutoka kwa Twaha Kassimu wa Morogoro wakati wa mpambano wao uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Kassim alishinda kwa K,O ya raundi ya 6
Bondia Cosmas Cheka kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Ramadhani Shauri wakati wa mpambano wao uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Cheka alishinda kwa point mpambano uho wa raundi 8.
Picha Zote na SUPER D BOXING NEWS

Sunday, December 21, 2014

NGOMA MPYA YA MOPLUS - WAFUNDISHE

Inline image 1
Bofya HAPA https://mkito.com/song/wafundishe/7941 kupakua wimbo wa Moplus aka Baba Wa Ukoo Kwa jina "WAFUNDISHE",ikiwa ni HipHop category

NGUNI KUPIGWA JANUARY 2 IFAKALA UKUMBI WA MAKUTANO IFAKARA


Na Mwandishi Wetu
MPAMBANO wa ngumi wa kufungua mwaka unatarajia kupigwa Ifakala mkoa wa morogoro kwa ajili yas kuhamasisha na kukuza mchezo wa masumbwi nchini akizungumza na waandishi wa habari promota wa mpambano huo, Hiari Bohari amesema kuwa kwa sasa anataka aendereza mchezo wa masumbwi Ifakala kwa kuwa watu wapo na mchezo unapendwa
aliongeza kwa kusema siku hiyo ya january mbili itakuwa ni siku ya kufungua mwaka kwa mpambano wa masumbwi kati ya Abdallah Kilima na Abdul Amwenye uku Saleh Makuka akipambanma na Said Chamak
vile vile kutakuwa na mpambano miwili kwa ajili ya kuamasisha wanawake waje washiriki katika michezi ya ngumi siku hiyo Aika Georger atapambana na Najma Ally
aliongeza kwa kusema anawaomba wadau mbalimbali kutoa sapoti na kumuunga mkono katika harakati za kuinua mchezo wa masumbwi ili uweze kusonga mbele

Friday, December 19, 2014

STEPS KUTAMBULISHA FILAMU KATIKA MUONEKANO MPYA KWA MWAKA 2015

Mratibu wa mpango mpya wa Steps Entertainment, myovela Mfwaisa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Mtayarishaji na mwongozaji wa Filamu nchini, Jackob Steven 'JB' akizungumzia ujio mpya wa Steps.
Wakionesha Makasha mapya ya muvi za kibongo zitakazoanza kusambazwa na Steps mwaka 2015

Na Mwandishi wetu
Kampuni ya usambazaji wa filamu bora Tanzania ya Steps Entertainment Ltd inatarajia kutoa bidhaa mpya za filamu kwa mwaka ujao wa 2015 filamu zenye ubora muonekano mzuri huku pia kuwaletea walaji bei rafiki kutoka kampuni bor a ya usambazaji wa filamu Tanzania Steps Entertainment Ltd.
Steps Entertaiment Ltd ni ilioanzishwa mwaka 2007 nchini Tanzania na makao yake makuu yako jijini Dar salaam, Kampuni ya Steps Entertainment inajishughulisha na usambazaji wa filamu za Kitanzania maarufu kwa jina la  BONGO MOVIES
Tangu kuanzishwa kwake Kampuni ya Steps Entertainment imekuwa mdau mkubwa katika kukuza tasnia ya filamu nchini Tanzania na mpaka sasa ndiyo kampuni kubwa ya usambazaji wa filamu nchini Tanzania. 
Kampuni ya Steps Entertainment kupitia mikakati yake ya kuinua tasnia ya filamu nchini Tanzaania imefanikiwa kutoa ajira nyingi kwa wadau mbalimbali wa tasnia ya filamu, wakiwemo waandaaji wa filamu, Waigizaji, Wasambazaji wakubwa kwa wadogo, Wauzaji wa rejareja na wanaoonyesha na au kukodisha katika vibanda. 
Akiongea na wanahabari Carlos Johns Silondwa mtendaji mkuu ameielezea Steps Entertainment imefanikiwa pia kuvuka mipaka na kufikisha sinema za kitanzania katika mataifa mbalimbali ya nje na katika luninga za kimataifa na televisheni za ndani kuonyesha kazi za nyumbani.
“Kwa sasa mataifa mengi Ulaya na nchi za Scandinavia wanajifunza Lugha yetu ya Kiswahili kupitia filamu zetu, moja kwa moja utaona njia nyingine katika kukuza Kiswahili nje ya nchi kwa njia ya filamu tu ambazo zinasambazwa na kampuni hii, na kutengeneza ajira kwa vijana wengi,”
Pia kampuni imekuja na bei rafiki kwa mlaji baada ya kilio chake kuumiza kwa muda mrefu, kampuni kwa kutumia wataalamu pamoja na wadau wa filamu kutoka sehemu mbalimbali wamefanya utafiti ili kupata Mwarobaini wa Maharamia wa kazi za nyumbani kampuni imeshusha bei.
Hiyo inatokana na hali halisi filamu inatakiwa imfikie mtumia kwa 6,000/ lakini utafiti umebaini kuwa mtanzania anatumia zaidi kiasi cha 34,000/ na zaidi bila kuimiliki Dvd hiyo, baada ya Vibanda au Library kuanzimisha, badala ya kumuuzia. 
Filamu ambayo itauzwa ikiwa katika ubora na muonekano mzuri, inakuja baada ya filamu kutoka nje, kuuzwa kwa bei ya chini kabisa na kuleta ushindani pamoja na kuwa sinema hizo hazilipiwi kodi tofauti sana, nakuzifanya zinunulike sana kuliko filamu za ndani kutokana na bei yake kuwa ndogo.
 Kampuni ya Steps Entertainment ilifanya utafiti ili kujua ni jinsi gani filamu zinatoka mbali na bado zinawafikia walaji kwa bei ya chini ni baada ya utafiti huo ndipo Kampuni ya Steps Entertainment iliamua kujibana na kufanikiwa kuingiza na kufunga mtambo mkubwa wakisasa kuzalisha cd/dvd, kuzirekodi na kuziprinti hapa hapa nchini.
Tofauti  na siku za nyuma ambapo ilikuwa inaagiza cd/dvd kutoka nje ya nchi na kuja kuzirekodi tu, sambamba na mtambo huo pia kampuni hii imeamua kubuni kifungashio kipya yaani kasha za cd/dvd, ambayo ni za bei nafuu, zinamuonekano mzuri zaidi, ni rahisi kuhifadhi, nirahisi kusafiriha na nirafiki wa mazingira.
Mtambo mkubwa na wakisasa pamoja na kifungashio kipya vimepunguza sana gharama za kuzalishia nakala za dvd na cd na hivyo Steps imeona ni vyema kuonyesha moyo wa uzalendo kwa wateja wake  kwa kuwapunguzia bei ya kununua filamu kwa kuwauzia kwa nusu ya bei ya awali.
Kampuni ya Steps Entertainment inaamini kuwa kitendo cha kupunguza bei za filamu zake, kitawanyima Maharamia ulafi na wizi wa wazi kabisa, kama kampuni inakaribisha wadau wote wanaosambaza filamu kwa kuja kwetu kuzalishiwa filamu zao kwa bei rahisi sana ili huyu Gaidi mkubwa anayenyonya kazi zetu aache. 
  • Kinaonyesha moyo wa uzalendo lakini pia kitapandisha mauzo ya filamu za kitanzania ambapo kwa ujumla wake itaongeza kipato kwa wasanii na kuchangia pato la Taifa.
  • Kitapunguza uharamia wa filamu kwa kuwa bei itakuwa chini hivyo kila mtu atakuwa na uwezo wa kununua nakala halisi.
  • Kitaziwezesha library zinazokodisha filamu kuacha kukodisha na badala yake kuanza kuuza moja kwa moja
 Hivyo basi Kampuni ya Steps Entertainment inamaliza mwaka 2014 na kuingia mwaka 2015 kwa kubororesha bidhaa zake, zikiwa katika ubora na muonekano wa kuvutia kwenye kasha la bahasha ngumu, bidhaa hizi zitamfikia mlaji kwa bei ya  1,500/= tu bei hii kwa filmu zitakazo kuwa katika kifungashio kipya pekee filamu zitakazo kuwa katika kifungashio cha zamani yaani kasha la plastiki zitaendelea kuuzwa kwa bei ile ile na wateja watakuwa huru kuchagua aina ya kifungashio pale wanaponunua nakala za filamu za Steps
Hivyo basi Steps Entertaiment imeanzisha kampeni maalum ya “Faidika na Steps kwa bidhaa bora, Wasanii nyota, na Filamu Bora”.
Kampuni ya Steps Entertainment  inawaomba wadau wote kuendelea kuzienzi filamu za kitanzania ili kukuza kipato cha wasanii na taifa kwa ujumla , kutangaza lugha ya Kiswahili na utamaduni wa kitazania.
Bei zetu zitakuwa wazi kwa maan za steps tofauti ya bei iliyoandikwa kwenye kasha ya kuonekana zikiwazimeandikwa katika kasha na mwananchi asikulaghai mtu wa Library eti usinunue hadi hakukodishe sema No.

Mwisho, Tunaiomba Serikali Chini ya Rais wetu Mpendwa Mheshimiwa Dr. Jakaya Mrisho Kikwete wawasaidie wadau wa filamu kupambana na uharamia wa filamu ambao kwa sasa umevuka mipaka wezi wanafanikiwa wasanii wanabaki Maskini.
MUNGU IBARIKI TANZANIA Mungu bariki Afrika 
Carlos Johns Silondwa 
Mtendaji Mkuu.


Tuesday, December 9, 2014

FAINAL YA MASHINDANO YA WAZI YA TAIFA YA NGUMI YALIVYO MALIZIKA MWISHONI MWA WIKI UWANJA WA NDANI WA TAIFA

Mabondia latifa Halidi  kushoto wa Kigoma na Vumilia Kalinga wa JKT wakioneshana umwanmba wa kutupiana makonde wakati wa mashindano ya taifa ya wazi yaliyomalizika mwishoni mwa wiki iliyopita
Makamu wa Rais wa Shirikisho la ngumi za Ridhaa nchini 'BFT' Lukelo Willilo akimvisha medali ya dhaabu bondia Robert Kyaruzi baada ya kushinda katika fainal ya mashindano ya taifa ya wazi iliyomalizika mwishoni mwa wiki iliyopita
Mabondia Siwatu Elieta kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Zulfa Macho wakati wa fainali za mchezo wa masumbwi Macho alishinda kwa point mpambano huo
Mabondia latifa Halidi  kushoto wa Kigoma na Vumilia Kalinga wa JKT wakioneshana umwanmba wa kutupiana makonde wakati wa mashindano ya taifa ya wazi yaliyomalizika mwishoni mwa wiki iliyopita

 Mfanya biashara na mdau na promota maarufu nchini Zahoro Maganga akisalimiana na bondia  wakati wa fainali ya mashindano ya taifa.
Picha zote na SUPER D BOXING NEWS

"OFFICIAL VIDEO' I SEE ME - JOH MAKINI

VIDEO MAKING OF I SEE ME - JOH MAKINI

Inline image 3Inline image 1Inline image 4Inline image 2Inline image 8Inline image 5

Monday, December 8, 2014

ILIVYOKUWA WAKATI IDRIS ANACHUKUA USHINDI WA BBA- HOT SHOT 2014


MSHIRIKI KUTOKA TANZANIA, IDRIS AIBUKA NA USHINDI KATIKA JUMBA LA BIG BROTHER AFRICA - HOT SHOT



Idriss

RAIS KIKWETE APANGUA TENA WAKUU WA MIKOA


Jakaya Kikwete, president of Tanzania, answers questions at a press conference at the United Nations (UN) building in Addis Ababa, Ethiopia, during the 12th African Union (AU) Summit.
Rais Jakaya Kikwete

Mwandishi Wetu
Dar es Salaam. Rais Jakaya Kikwete amempandisha cheo Mkuu wa Wilaya ya Karatu, Daudi Ntibenda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha na kuwahamisha vituo vya kazi wakuu wengine sita wa mikoa kuanzia jana.
Taarifa iliyotolewa jana na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue ilisema Ntibenda ataapishwa leo, saa nne asubuhi, Ikulu, Dar es Salaam.
Wakuu wa mikoa waliohamishwa ni Elaston Mbwilo anayetoka Manyara kwenda Simiyu kuchukua nafasi ya Paschal Mabiti aliyepewa likizo ya ugonjwa.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera anahamia Manyara kutoka Morogoro na nafasi yake inachukuliwa Dk Rajabu Rutengwe kutoka Tanga alikokaa kwa mwezi mmoja akitokea Katavi.
Magalula Magalula amehamishiwa Tanga kutoka Lindi ambako naye alikaa kwa mwezi mmoja akitokea Geita na nafasi yake inazibwa na Mwantumu Mahiza kutoka Pwani.
Mhandisi Evarist Ndiliko amehamishiwa Pwani kutoka Arusha alikohamia hivi karibuni kutoka Mwanza.
Katika taarifa yake, Balozi Sefue alisema wakuu wengine wa mikoa wanaendelea kubakia katika vituo vyao vya sasa vya kazi.
Uhamisho huo umekuja ikiwa ni mwezi mmoja kamili tangu Rais Kikwete alipofanya uteuzi wa wakuu wapya wanne wa mikoa na kuwahamisha sita huku wengine watatu wakipangiwa kazi nyingine.
Wakuu wa mikoa wanne wapya ni Dk Ibrahim Msengi (Katavi), Amina Masenza (Iringa), Halima Dendego (Mtwara) na John Mongella (Kagera).
Kabla ya kuteuliwa, Masenza alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Mwanza; Dk Msengi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Kilimanjaro na Mongela alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha.
Walioachwa kwa ajili ya kazi nyingine ni Dk Christine Ishengoma (Iringa), Kanali Fabian Massawe (Kagera) na Kanali Joseph Simbakalia aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, ambaye tayari ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maeneo Maalumu ya Uwekezaji kwa Mauzo ya Nje (EPZA).
Sorce- gazeti la Mwananch 08/12/2014

Wednesday, November 19, 2014

MDAU ANDREW CHALE KUTOA VITABU VYA MAISHA YAKE

Andrew Chale (kulia) akiteta jambo na 'Mwenyekiti'  Maggid Mjengwa wa Mjengwa Blog.
================================

Na Mwandishi Wetu
Mwandishi wa Habari nchini Tanzania, Andrew Chale anayeandikia magazeti ya Tanzania Daima na Sayari yanayotolewa na kampuni ya Free Media ya jijini Dar es Salaam, ambaye pia mwandishi 'msaada' wa blog za habari mbalimbali za hapa nchini na nje ya Tanzania ameanza mchakato rasmi wa kuandika vitabu  vitatu (3) vitakavyokuwa vikielezea juu ya Maisha yake.
Katika taarifa yake aliyoitoa kwa vyombo vya habari leo Novemba 19,  Andrew Chale alibainisha juu ya kusudio hilo  la kutoa Vitabu  vya kuelezea Maisha yake ni ndoto aliyonayo kwa miaka mingi na kwa sasa imetimia.
"Wengi watajiuliza sasa nimepata wapi ujasiri wa kufanya jambo hili kubwa la kuelezea Maisha yangu?.Ni rahisi sana, Unapokuwa na Mungu kila jambo linawezekana hivyo vitabu hivi vitakuwa ni muongozo kwa Vijana wote hapa Duniani kuelewa kuwa yale yote wanayopitia si ya kuyakatia tamaa, bali kuangalia wapi wataweza kujikomboa na hata kuendana na hali iliyopo kwa kujithamini, kujielewa, uvumilivu na kufikia malengo stahiki ya maisha" alifafanua Andrew Chale.
Alivitaja vitabu hivyo kuwa ni: "Who Is Andrew Chale?" Sehemu ya Kwanza), 'Who Is Andrew Chale 2?"- 'Nimnukuu Nani?' (Sehemu ya Pili)  na Kitabu cha mwisho kitakachojulikana kama "Mimi ni Historia".
Akifafanua vitabu hivyo vya 'Who Is Andrew Chale' cha kwanza na kile cha pili cha 'Who Is Andrew Chale 2- 'Nimnukuu Nani?', alibainisha kuwa vitaelezea kwa kina Historia yake tokea kuzaliwa hadi alipofikia sasa huku cha Pili cha 'Who Is Andrew Chale 2-'Nimnukuu Nani' kikielezea yale mambo yote yaliyojificha nyuma ya pazia na ukakasi wa maisha aliyopambana nayo kutoka kwa walimwengu na mwishowe anauliza "Nimnukuu Nani?".

Aidha, kwa upande wa kitabu cha : "Mimi ni Historia" ameweza kuelezea ujumbe juu ya Vijana kutokata tamaa na baadala yake wasonge mbele kwa magumu yote waliyopitia, ikiwemo yeye.
"Mimi ni Historia", mimi mwenyewe naogopa sana, kwanza kuanzia jina la Kitabu, Nakumbuka nilimuuliza Mama yangu Mzazi juu ya jambo fulani la kifamilia baina yake na Baba,  lakini jibu alilonipa ndilo lililonifanya nishike neno hili 'Mimi ni Historia'. Kikubwa kwenye kitabu hichi nitafafanua mambo mbalimbali ya kihistoria  bila shaka hata atakayesoma ambaye alipitia mambo kama yangu naye itakuwa ni Historia" alimalizia Andrew Chale.
Vitabu hivyo vyote vitajaa Historia ya kweli, itakayotoa mafunzo kwa kila mmoja atakayebahatika kuvisoma Pia vitakuwa ni kama mafunzo, mfano wa kuigwa, na kukuacha ki mdomo wazi na hata kububujikwa machozi.
Aidha, Andrew Chale, aliomba ushirikiano kwa wadau kujitokeza kumsapoti ilikufanikisha juhudi za vitabu hivyo ikiwemo gharama za kuandaa Mswada, mapitio na uchapaji.
"Kwa sasa nipo katika andalio la Simulizi, na lengo kuu nije nichapishe Mkuki na Nyota.Kwa sasa natafuta watu watakao kuwa msaada wa awali wa kufanikisha dhumuni langu hili Ikiwemo ushahuri, msaada wa kifedha, mchango wa kimawazo na mengineo. Tuwasiliane kupitia 0719076376 au 0767076376 au 0688076376 au chalefamily@yahoo.com" alimalizia Andrew Chale.
Andrew Chale, ambaye kwa sasa anaishi Bagamoyo, Mkoani Pwani akifanya shughuli zake hizo za Uandishi wa Habari, Pia ni Mwanaharakati wa Haki za Watoto nchini, msanii wa masuala ya Vichekesho, Mtunzi wa filamu, maigizo na mshahuri kwenye matamasha ya sanaa na Muziki, mbali hayo pia ni Mjasiriamali katika Sanaa na Utamaduni ikiwemo kukuza Sanaa na Utamaduni kwa Mkoa wa Pwani.

BASATA NA KITUO CHA UTAMADUNI CHA UJERUMAN (GOETH INSTITUT) WAENDESHA MAFUNZO KWA WASANII WA SANAA ZA MIKONO

Kaimu Katibu Mtendaji wa BASATA Godfrey Mngereza (Kushoto) akisisitiza jambo wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wasanii wa batiki yaliyoanza mapema wiki hii kwenye Ofisi za Baraza hilo zilizoko Ilala Sharif Shamba jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Kituo cha Utamaduni cha Ujereum Bi. Eleonore Sylla na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Maendeleo ya Utamaduni  Bi. Leah Ruhimbi

Mkurugenzi wa Kituo cha Utamaduni cha Ujereum Bi. Eleonore Sylla akiongea na Wasanii (hawako pichani) waliohudhuria kwenye mafunzo ya wiki moja ya utengenezaji batiki yanayoandaliwa na kituo chake kwa kushirikiana na BASATA na kufanyika makao makuu ya BASATA. Mwingine katika picha ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Maendeleo ya Utamaduni Bi. Leah Ruhimbi
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Maendeleo ya Utamaduni Bi. Leah Ruhimbi akifungua mafunzo ya utengenezaji batiki kwa wasanii wa Sanaa za Ufundi yanayofanyika kwa wiki moja makao makuu ya BASATA Ilala Sharif Shamba. Wengine kutoka kulia ni  Mkurugenzi wa Idara ya Ukuzaji Sanaa kutoka BASATA Bi. Vivian Shalua na Mkurugenzi wa Kituo cha Utamaduni cha Ujereum Bi. Eleonore Sylla
Mkurugenzi wa Idara ya Ukuzaji Sanaa kutoka BASATA Bi. Vivian Shalua akiwaelekeza jambo wasanii wanaoshiriki mafunzo ya utengenezaji batiki 
Sehemu ya Wasanii wa utengenezaji batiki wakifuatilia kwa makini mafunzo hayo.
=======================================

Na Mwandishi Wetu
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kwa kushirikiana na Kituo cha Utamaduni cha Ujeruman maarufu kama Goeth Insitut wameendesha mafunzo ya utengenezaji batiki kwa wasanii wa Sanaa za mikono yanayofanyika kwenye Ukumbi wa BASATA jijini Dar es Salaam.
Mafunzo hayo yanayotazamiwa kudumu kwa siku tano yaani kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa yanalenga kuongeza ubunifu na weledi miongoni mwa wasanii wa Sanaa za mikono ili kuongeza ubora na tija katika uzalishaji.  
Mapema akizungumza kwenye uzinduzi wa mafunzo hayo, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Maendeleo ya Utamaduni chini ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Leah Ruhimbi alisema kwamba mafunzo hayo yatasaidia kuongeza tija kwa wasanii hao na kuwawezesha kubuni Sanaa zenye ubora zitakazopenya masoko mbalimbali ya Sanaa.
“Ni matarajio ya BASATA na wizara kwamba mafunzo haya yatakuwa yenye tija kwa wasanii na yatawawezesha kusambaza ubunifu na uzoefu kwa wasanii wengine nchini. Lengo ni kuwa na sanaa zenye ubunifu na ubora” alisisitiza.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Goeth Institut Bi. Eleonore Sylla alisema kwamba mafunzo hayo yanahusisha wasanii wenye uwezo wa kutengeneza batiki na lengo kuu ni kuwaweka pamoja ili wachangie uzoefu na baadaye kutengeneza batiki zenye ubora zaidi.
“Tunajua mnatoka sehemu mbalimbali nchini na wote mna uzoefu katika utengenezaji wa batiki lakini kuwa kwenu pamoja kwenye mafunzo haya kutawafanya mpate uzoefu zaidi na hatimaye kubuni batiki zenye ubora” aliongeza Sylla.
Naye Kaimu Katibu Mtendaji wa BASATA Godfrey Mngereza alisema kwamba BASATA kwa kushirikiana na Goeth Insitut wameona kwamba kuna haja ya mafunzo hayo ya wasanii na kwamba baraza litaendelea kuboresha ubora wa kazi za Wasanii kupitia kuwajengea uwezo.


Sunday, November 2, 2014

MABONDIA WAZIPIGA MAZOEZINI WAKISIMAMIWA NA KOCHA SUPER D

Bondia Shabani Kaoneka kulia
akimtupia konde  Obago Kamata wakati wa mazoezi yaliyofanyika shule ya uhuru uwanja wa basket yakisimamiwa na Super D Boxing Coach Dar es salaam

Bondia Shabani Kaoneka kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Obago Kamata wakati wa mazoezi yaliyofanyika shule ya uhuru uwanja wa basket yakisimamiwa na Super D Boxing Coach Dar es salaam
Bondia Jumaa Rashid akioneshana ubavu na Juma Biglee wakati wa mazoezi yaliyofanyika katika uwanja wa shule ya uhuru uwanja wa basket yaliyokuwa yakisimamiwa na Super D Boxing Coach Dar es salaam.
Bodia Obaga Kamata kushoto akipambana na Idrisa Mweta wakati wa mazoezi yaliyofanyika shule ya uhuru uwanja wa basket yakisimamiwa na Super D Boxing Coach
Bondia Omari Bai kushoto akipambana ya Kelvin Majiba wakati wa mazoezi yaliyofanyika katika uwanja wa basket shule ya uhuru yaliyokuwa yakisimamiwa na Super D bOXING coach Dar es salaam juzi.
Picha zote na SUPER D BLOG

Monday, October 13, 2014

NGUMI KALI KUPIGWA OCTOBA 25 KATIKA UKUMBI WA FRIENDS CORNER MANZESE


Na Mwandishi Wetu
MPAMBANO wa mchezo wa masumbwi mkali utakaokutanisha mabondia mbalimbali kutoka kila kona ya Tanzania utafanyika
October 25 katika ukumbi wa friends Corner manzese jijini Dar es salaam akizingumza na waandishi wa habari mratibu wa mpambano huo kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D'
amesema kuwa siku hiyo kutakuwa na mpambano wa mahasimu katika mchezo wa ngumi kati ya bondia Saidi Mbelwa 'Moto wa Gesi'  na George Dimos mpambano mwingine utawakutanisha Amani Bariki 'Manny Chuga' na Ally Bugingo mpambano unaosubiliwa kwa hamu kila kona ya jiji la Dar es salaam ambapo mabondia hawo wamejizolea umaarufu mkubwa kupitia mchezo huo
pambano jingine ni kati ya Juma Fundi atakaezichapa na Hamza Mchanjo wakati Hasani Mandula ataonyeshana kazi na Mohamedi Jaka na Shabani Kaoneka atazipiga na Ibrahimu Maokola anaejiandaa kuwania kucheza ubingwa wa taifa mwishoni mwa mwaka huu Fadhili Boika atazipiga na Godfrey Silver  na Habibu Pengo atazidunda na Abdallah Luanje, Kashinde Mohamedi atazidunda na Mohamed Kibaga wakati Sadiki Nuru atakumbana na Mohamed Mbishi
katika mpambano huo siku hiyo kutakuwa na ulinzi wa kutosha kabisa kutokana na kujipanga vizuri katika swala hilo  kingilio ni shilingi, 5000; kwa kila mtu mchezo huu utapambwa na burudani mbalimbali siku hiyo pia kutakuwa zikiuzwa DVD mpya za masumbwi ambazo zinaonesha mafunzo mbalimbali ya mchezo wa ngumi yanavyoanza hatua kwa hatuampaka kujua kitu kamili katikamchezo huo pia kunakuwa na mapambano ya mabondia mabigwa wa dunia wa mchezo huo kama Floyd  Maywether, Manny Paquaio,mike Tyson, Mohamed Alli pamoja na mabambano ya ngumi ya ndani
Kwa Hisani ya :-

Wednesday, October 1, 2014

SIKILIZA NA KUPAKUA WIMBO MPYA WA METTY Ft CONRAD - NAJUA

Chek HAPA- http://www.hulkshare.com/sulejr/metty-najua-1 kupakua wimmbo mpya wa Metty - NAJUA. Ngoma imefanyika katika studio za Cenrirc Record akiwa amemshirikisha msanii Conrad. kwa mahojiano/mawasiliano zaidi check na Metty kwa nambari +255 714796622 powered by www.mtotowakitaa.blogsport.com