b..

B1

Wynem

animation

Thursday, June 16, 2016

MABONDIA GALILE NA MAPAMBANO KUMALIZA UBISHA JULAY 24 MUSOMA BAR

Mdau wa masumbwi nchini Jumanne Mbwembwe akiwainua mikono juu mabondia Imani Mapambano kushoto na Seleman Galile kwa ajili ya kutambulisha mpambano wao wa julay 24 katika ukumbi wa musoma bar Tandika 
Mabondia Iani Mapambano kushoto na Selemani Galile wakiwa katika pozi wakati wa utambulisho wa mpambano wao wa julay 24 katika ukumbi wa musoma bara tasndika
Mabondia Imani Mapambano kushoto akitunishiana misuli na Selemani Galile baada ya kusaini mkataba wa kuzipiga julay 24 katika ukumbi wa musoma bar tandika

Na Mwandishi Wetu
MABONDIA Imani Mapambano na Selemani Galile wamesaini mkataba wa kuzipiga Julay 24 katika ukumbi wa musoma bar uliopo tandika Dar es salaam
akizungumza baaya kusainishwa kwa mabondia hawo mratibu wa mpambano uho Rajabu Mhamila 'Super D' 
Amesema amewasainisha mabondia hawo baada ya kutambiana mara kwa mara kadri wakutanapo
hivyo 
nimeamua wapambane julay 24 katika ukumbi wa musoma bar ili kumaliza ubisha wao 
mpambano uho utakuwa wa ubingwa wa Taifa utakaosimamiwa na TPBO chini ya rais wake Yassin Abdallah 'Ustadhi' 
Aliongeza kwa kusema kuwa mipambano mingine ya utangulizi watatangaza kadri watakavyo ingia mikataba na mabondia mbali mbali  

Katika Mchezo huo kutakua na Uuzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi pamoja na kutambua sheria zake mbalimbali zitakazokua zikisambazwa na kocha wa mchezo huo mkoa wa kimichezo wa Ilala Rajabu Mhamila 'Super D' kwa ajili ya kuwapa mambondia mbalimbali mbinu za mchezo na mashabiki kujua sheria za masumbwi.


Ndani yake wakiwemo mabondia Floyd Mywether, Manny Paquaio, Amiri Khani, Mohamedi Ali, Mike Tayson David Haye na wengine ambapo kutakuwa na matukio ya mazoezi yao katika mataifa yao ikumbukwe kuwa ni mabingwa wa dunia. na kutakuwa na mapambano makubwa matano ya utangulizi

Friday, June 3, 2016

NGUMI ZA KIMATAIFA KUPIGWA KESHO UWANJA WA NDANI WA TAIFA JUNI 4

Mabondia Vicent Mbilinyi kushoto akitunishiana misuli na Msafili Haule baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambao wao utakaofanyika katika uwanja wa ndani wa Taifa siku ya jumamosi ya juni 4.
Promota wa mkanda wa ubingwa wa Dunia wa U.B.O Juma Ndamile kushoto akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kutangaza mpambano uho pamoja na upimaji uzito kwa mabondia wengine ni Kulwa Makaranga na bondia Cosmas Cheka atakaegombania ubingwa wa Dunia na Chrispin Moliyati mpambao wao utakaofanyika katika uwanja wa ndani wa Taifa siku ya jumamosi ya juni 4.
Bondia Lulu Kayage kushoto akitunishiana misuli na mpinzani wake Will Enelesi wa Malawi mpambano wao utafanyika juni 4 katika uwanja wa ndani wa Taifa 
Bondia Ashiraf Selemani kutoka Zanzibar  kushoto akitunishiana misuli na ElickGogodo wa Malawi baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao utakaofanyika kesho katika uwanja wa ndani wa Taifa.
Bondia Alphonce Mchumiatumbo kushoto akitunishiana misuli na Mussa Ajiba baada ya kupima uzito kwa ajili ya Mpambano wao utakaofanyika kesho katika uwanja wa ndani wa Taifa
Mabondia Vicent Mbilinyi kushoto akitunishiana misuli na Msafili Haule baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambao wao utakaofanyika katika uwanja wa ndani wa Taifa siku ya jumamosi ya juni 4
Mabondia Vicent Mbilinyi kushoto akitunishiana misuli na Msafili Haule baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambao wao utakaofanyika katika uwanja wa ndani wa Taifa siku ya jumamosi ya juni 4 

Picha zote na SUPER D BOXING NEWS



Na Mwandishi Wetu
BONDIA Cosmas chka anapanda uringoni kugombania ubingwa wa Dunia wa U.B.O kwa kupambana na Chrispin Moliyati kutoka Malawi mpambano wa raundi 12 wakisindikiza na mabondia chipkizi ambapo bondia kutoka katika kambi ya 'Super D' Vicent Mbilinyi ata kabiliana na bondia kutoka kambi ya akina ukoo wa Matumla Msafili Haule watazipiga katika uzito wa kg 63 mpambano wa raundi 6.
Mipambano mingine ya kimataifa yaa wakutanisha mabondia wa kike Lulu Kayage wa Tanzania atakaezipiga na Will Eneles kutoka Malawi
wengine ni Japhert Kaseba atazidunda na Amour Mzungu kutoka Zanzibar na Ashiraf Selemani kutoka Zanziba atakumbana na Elick Gogodo wa Malawi katika mchezo wa uzito wa juu kabisa wakati Alphonce Mchumiatumbo atakabiliana na Mussa Ajibu kutoka Malawi mpambano wa raundi sita

siku hiyo kutakuwa na burudani mbalimbali zitakazo sindikiza mapambano hayo ya kimataifa ya mchezo wa masumbwi pia ngumi zitaanza mapema kuepusha usumbufu unaojitokezaga kwa wapenzi kuchelewa majumbani mwao kwa ajili ya mchezo wa masumbwi

siku hiyo pia kutakuwa na ugawaji wa zawadi kwa mabondia watakaocheza vizuri na kuonesa nidhamu ya mchezo wa masumbwi ikiwemo vifaa vya mchezo pamoja na DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi pamoja na kutamba sheria za mchezo uho nyingine zitakuwa zikiuzwa kwa galama nafuu kwa mashabiki watakaofika siku hiyo.