b..

B1

Wynem

animation

Monday, January 26, 2015

MASHAIRI YA WIMBO WA 'BONGO HIP HOP' WA FID Q FT P FUNK MAJANI


VERSE 1:
Ulianza wewe.. wakaja waimbaji na wabana pua/
Wale mwewe.. Franga wawindaji wakatusua/
Kwakuwa.. wanajua mshikaji unaishi kwa miko/na zako itikadi.. ziko kimziki na sio mshiko/
Kama haileti hela..basi haimake sense.. no sweat kisela mie nikakomaa tu na lako penzi/
Sikusound garbage au kuchange suddenly../
Mie ni mjeshi so naweza fight savagely/
Hiphop ya ukweli.. ukapigwa radioni/sometimes malaika wa heri nao hutembelea motoni/
Penzi ni kipofu na anayemuona halioni/ sikuwa na hofu.. mama alinipenda tangu nikiwa tumboni/
I started young.. I made my mother's womb a drum/
My umblirical chord a guitar.. muhoji aliyenizaa/
BONGOFLAVA mzuri kiasi.. hiphop we ndo my queen/ my 1st.. my last & everything in betweenjj


Chorus:
Mimi na wewe.. tangu long time/ Kabla ya hizi pesa kabla haijaja hii Fame/
Cha ajabu haujabadilika na upo kwenye mainstream… BONGO HIPHOP X2

VERSE 2:
Kama kukupenda wewe ni dhambi.. basi shetani yu nami/ na kamwe sintonyea kambi ili niwabambe dukani/
For a million little pieces naweza kumcon Oprah ka James Frey/
Na watasema sitishi wakati wanaogopa nisitokee/
Waufuate mkumbo huu wa wasomi.. wa midundo na mistari/ ukiwa na nyundo mkononi.. ni rahisi kupigilia msumari/
Sio tu bongo.. mpaka Ng'ambo hakuna uhuru wa habari/ kuna uhuru wa mwenye chombo.. mitambo na mwenye mali/
Kujifanya hawasikii.. haiwasaidii.. wala haiwajengi/ unachosema ni.. kamwe IPP haitompinga Mengi/
Unawakumbusha wazazi wa uswazi.. chati ya uteja imeingia/ na Mapusha wanauza drugs ili walishe familia/
Mbaya.. kuhifadhi fuvu la mtu ndani ya kabati/ mbaya zaidi ni kuwa na ndugu.. halafu kichwa maji/
Amka bongo lala.. hiphop sio ufala.. ni lazima uifate/
Uaminifu ni kama mshahara.. fanya kazi ili uupate

Chorus:
Mimi na wewe.. tangu long time/ Kabla ya hizi pesa kabla haijaja hii Fame
Cha ajabu haujabadilika na upo kwenye mainstream… BONGO HIPHOP X2

VERSE 3:
Mapenzi ya sikuhizi.. bila kugombana yanakua hayana stimu/
Pia ni ruksa kushikana lakini sio kushikiana simu/
Inanipa wazimu.. kusikia kimwana haujaachana na Hasheem/
Na bado mnawasiliana..una mpango wa kuchanganya timu?/
Nakupenda hiphop.. ndo maana ninarap ile mbaya/
Naspit fire bila hennessy.. au kula kaya/
I want my art to be my legacy.. kabla sijaretire.. waanze nigwaya hawa enemies.. anyways NI HAYO TU/
Beef huletwa na wivu.. na wivu sio hiphop/

Chorus:
Mimi na wewe.. tangu long time/ Kabla ya hizi pesa kabla haijaja hii Fame/
Cha ajabu haujabadilika na upo kwenye mainstream… BONGO HIPHOP X2

Monday, January 19, 2015

"NEW AUDIO" BARAKAH DA PRINCE - SIACHANI NAWE

Kwa kusikiliza na kupakua wimbo mpya wa Baraka Da Prince - SIACHANI NAWE.

Thursday, January 15, 2015

HASHIM KAMBI KUONGOZA NYOTA BONGO KATIKA FILAMU YA CPU




Na Mwandishi Wetu
MSANII mkongwe katika tasnia ya filamu Swahilihood Hashim Kambi 'Ramsey’ ni moja kati ya wasanii wakubwa Bongo ambaye atawaongoza wasanii nyota na wakongwe katika filamu kubwa ya CPU inayotarajiwa kuingizwa katika Dvd baada ya kuonyeshwa katika majumba ya sinema ndani na nje ya Bongo.
Filamu ya CPU ni kazi kubwa sana kutengenezwa na watayarishaji wa ndani na kushirikisha wasanii zaidi ya mia mbili ndio filamu kubwa yenye ubora wa kipekee awali ilionyeshwa katika ukumbi wa sinema Century Cinemax Mlimani City kwa siku kumi mfululizo na kuacha gumzo kwa wapenzi wa sinema.
Kwa mara ya kwanza itauzwa katika Dvd ili kwa wale wapenzi wa filamu walioshindwa kuingia katika majumba ya sinema ilipoonyeshwa waweze kushuhudia teknolojia ya juu kutumika Bongo na kuwavutia wengi mtaani kwetu ambako ndio soko la filamu za kibongo lipo.
CPU inawakutanisha wasanii nyota na wakongwe ka aKulwa Kikumba ‘Kulwa Kikumba ‘ Dude’, Richard Mshanga ‘Masinde’, Dotnata, na nyota wengine kibao ambao wanafanya vizuri katika tasnia ya filamu wakiongozwa na Hashim Kambi ‘Ramsey’ msanii aliyejijengea mashabiki wengi.