b..

B1

Wynem

animation

Friday, October 25, 2013

Thursday, October 24, 2013

KICHUPA CHA MWANAMBUZI KIPO TAYARI, MDAU KAA MKAO WA KUKITAZAMA SIKU YEYOTE KUANZIA LEO

Video hii ya wimbo wa Mwanambuzi ulioimbwa na msanii Wynem, imefanyika katika production ya Sule's Inc. Chini ya Director, Sule Junior (Salum Suleiman)

Thursday, October 17, 2013

BONDIA, CHUGA BOY ALIVYO MSAMBALATISHA ISMAIL KAJIMA


Bondia Amani Bariki 'Chuga Boy' kushoto akipambana ya Ismail Kajima wakati wa mpambano wao uliofanyika Mbezi kwa Msuguli katika ukumbi wa Samunge Dar es salaam siku ya kusherehekea sikukuu ya Idi Chuga boy alishinda kwa pointi.

Bondia Amani Bariki 'Chuga Boy' akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Ismail Kajima wakati wa mchezo wao uliofanyika mbezi kwa msuguli ukumbi wa Samunge Dar es salaam wakati wa kusherehekea sikukuu ya Idi Chuga Boy alishinda kwa point mchezo huo.

Chuga Boy akitangazwa mshindi wakati wa mpambano huo
Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Wednesday, October 2, 2013

MPAMBANO WA MASUMBWI KUFANYIKA PANANDI PANANDI ILALA OKTOBA 26


Kocha wa Ngumi Rajabu Mhamila 'Super D' (kushoto) akiwaelezea jambo masahabiki wa mchezo wa ngumi kuhusu DVD zinazoonyesha mafunzo mbalimbali ya Mchezo huo.

Na Mwandish Wetu

MPAMBANO mwingine wa masumbwi kufanyika katika ukumbi wa panandi panandi Oktoba26 mpambano huo wa mchezo wa masumbwi utakaokuwa chini ya uratibu wa Kinyogoli Fondition utawakutanisha mabondia mbalimbali wenye majina na wanaotamba kwa sasa katika anga za masumbwi nchini.
Akizungumzia mchezo huo kocha wa Kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini kutoka kambi ya ilala Rajabu Mhamila 'Super D' amesema kuwa mpambano huo utawakutanisha bondia Yakubu Maganga atakae zichapa na Ubwa Salumu katika uzito wa kilo 75 huku Seif Ali akipambana na Hassani Labanda pamoja na mipambano mengine ya masumbwi itakayo wakutanisha mabondia mbalimbali Siku hiyo kutakuwa pia na huzwaji wa DVD kali za ngumi wakiwemo mabondia wakali wanaotamba Duniani na hapa nchini kama.Manny Paquaio, Saul 'canelo' alverez ,Floyd Mayweathar,Mike Tyson,Mohamed Ali,Ferex Trinidad,Miguel Cotto na wengine wengi.
DVD hizo za ngumi kali zitakuwa zikiuzwa na kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D'
Pamoja na kutambua sheria na taratibu za mchezo huo siku hiyo pia kuta kuwa na vifaa vya mchezo huo wa masumbwi vitakavyotolewa  zawadi kwa mabondia na Kocha Super D  ambaye ame haidi kutoa, Gum Shit ,Clip Bandeji,DVD za Mafunzo kwa mabondia, Bukta,Protector na vifaa mbalimbali kwa mabondia watakao onesha uwezo wa ali ya juu wa kutupiana masumbwi